SERIKALI KUIMARISHA SEKTA YA SHERIA NA HAKI ZANZIBAR; ZAIDI YA BILIONI 13.6 ZAWEKEZWA
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Mhe. Hemed Suleiman Abdulla, amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar itaendelea kuimarisha sekta ya sheria na haki ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma za haki kwa wakati, usawa na uwazi. Akizungumza katika maadhimisho ya miaka 24 ya kuanzishwa kwa Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka Zanzibar (DPP) yaliyofanyika Hoteli ya Madinat Al Bahr, Chukwani, amesema Serikali imetenga zaidi ya shilingi bilioni 13.6 katika mwaka wa fedha 2025/2026 kwa ajili ya kuboresha mahakama, mifumo ya TEHAMA na huduma nyingine muhimu zinazolenga kuongeza ufanisi wa utoaji haki. Mhe. Hemed amesema mafanikio ya mfumo wa haki jinai yanatokana na ushirikiano wa taasisi mbalimbali ikiwemo Mahakama, Jeshi la Polisi, Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka, TAKUKURU pamoja na wadau wengine wa sekta ya sheria. Aidha, ameipongeza Ofisi ya DPP kwa kuanzisha mfumo wa kidijitali wa "Ongea na DPP", uliorahisisha mawasiliano kati ya wananchi na taasisi hiyo. Kwa upande wake, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora, Mhe. Haruna Ali Suleiman, amesisitiza umuhimu wa kuimarisha ushirikiano wa taasisi katika mapambano dhidi ya dawa za kulevya. Naye Mkurugenzi wa Mashtaka Zanzibar, Ndugu Mgeni Jailani Jecha, amesema ofisi hiyo itaendelea kusimamia utekelezaji wa sheria kwa kuzingatia haki, usawa na maslahi ya wananchi. #Zanzibar #DPPZanzibar #Haki #Sheria #UtawalaBora #HemedSuleiman #ASAMOnlineTV #TrendingNow

WAZANZIBAR SIO WABAGUZI - DK MUCHUNGUZI, AFUNGUKA MAZITO

OMO ATOA DARASA MBELE YA RAIS MWINYI NA DKT SAMIA HII NI HISTORIA KWA UPINZANI

KIVUMBI NA JASHO WANANCHI WATOA YA MOYONI BAADA TAMKO LA SERIKALI KUHUSU RUSHA ROHO ZANZIBAR.

UCHAGUZI WA SERIKALI YA WANAFUNZI HORIZON INSTITUTE OF TECHNOLOGY

DC SAID HAJI MRISHO AKAGUA KARO LINALOVUJISHA MAJI MACHAFU FORODHANI

PROGRESS IN THE CONSTRUCTION OF PEMBA INTERNATIONAL AIRPORT.

HARUSI YA KIJESHI JKU

Presents President Samia with the Jeep driven from Oman to Tanzania, purchased for over 100 Million

MAKAMU WA PILI WA RAIS ASEMA SASA FIDIA ZILIPWE

FUNDI BOMBA AFARIKI KWA AJALI YA PIKIPIKI ALITIWA KAZI YA HARAKA

WANANCHI WAPONGEZA MARIDHIANO YA CCM NA ACT WAZALENDO, WASEMA NI MSINGI WA AMANI NA MAENDELEO

Rais Mwinyi leo amtumbua Mkurugenzi wa ZRB

MSIKITI NA KANISA ZANZIBAR VYAFUNGWA

MWANA FA APINGWA BAADA YA KUITAJA SERIKALI YA AWAMU YA 6, AJIBU: "TUNAJENGA ARENA!"

BREAKING: U.S. launches additional strikes on Iran as Strait of Hormuz standoff escalates

ZAIDI YA NCHI 20 KUSHIRIKI KONGAMANO LA KIMATAIFA LA MAFUTA, NISHATI NA GESI ZANZIBAR

WAWILI WAFARIKI BOTI IKIWAKA MOTO NDANI YA ZIWA VICTORIA -TASAC YAONGOZA OPERESHENI UOKOZI

Iran yatangaza kufungwa kamili kwa Hormuz

#ASAMLIVE: TAMKO LA PAMOJA LA MARIDHIANO YA KISIASA ZANZIBAR

