DC SIMALENGA AFUNGUA MAFUNZO YA SIKU MBILI YA MADIWANI 48 BARIADI DC NA BUSEGA DC

Madiwani Bariadi DC na Busega DC wasisitizwa uwajibikaji kwa wananchi. Rai hiyo imetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Bariadi Mhe. Simon Simalenga wakati wa Ufunguzi rasmi wa mafunzo elekezi kwa madiwani 48 kutoka Bariadi DC na Busega DC. Aidha Mkuu wa Wilaya ya Busega Mhe. Faiza Salim wakati wa ufungaji wa mafunzo hayo amewasisitiza kutumia maarifa waliyopata Madiwani hao kuwaletea wananchi maendeleo na kutatua changamoto zao.