Haleluya, Haleluya - TMW 110

TUMWABUDU MUNGU WETU YESU AMEFUFUKA Title: Haleluya, Haleluya Author: J.B. Dykes, & C. Wordsworth Music played by: Rev. Allan Kingu MANENO YA WIMBO: 1. Haleluya, Haleluya, Sauti na mioyo juu, tumwimbie Mungu nyimbo, tumsifu na furaha, Aliyemwaga damuye kwa ulimwengu wote, amefufuka kifoni sasa Yesu Mwokozi. 2. Minyororo yake kifo imekatika pia, na katika wafu wote Yee mzaliwa wa kwanza Yesu ameshinda sasa, nasi twashinda naye. Ametupatia nasi uzima wa milele. 3. Kristo afufuka kwanza nao wengi baadaye. Atakapokuja tena, watatokea naye, mavuno yatakuwako mwisho wa ulimwengu, watafika furahani wote watakatifu. 4. Mwokozi amefufuka, nasi tutafufuka. Tunyeshee kama mvua neema yako ee Bwana. Tutafute yaliyo juu, siyo ya ulimwengu, na uzima tutapewa naye Kristo kwa Mungu. 5. Tumsifuni, tumsifuni Mungu wetu, apaswa. Tumsifuni na Mwokozi, aliyeshinda vita. Tumsifuni naye Roho, kisima cha mapenzi. Tumsifuni Mungu wetu, ni Utatu wa enzi.