RAIS MWINYI ASISITIZA MATUMIZI YA TEHAMA KATIKA MAHAKAMA KUHARAKISHA UTOAJI WA HAKI

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amesema matumizi ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (Tehama) katika mfumo wa utendaji wa Mahakama ni eneo muhimu linalopaswa kupewa kipaumbele ili kuharakisha upatikanaji wa haki na kuongeza ufanisi wa utoaji wa huduma. Rais Dkt. Mwinyi ameyasema hayo leo, Juni 22, 2026, alipokutana na Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Jaji George Masaju, aliyefika Ikulu Zanzibar kwa ajili ya kujitambulisha. Amesema Mahakama ya Zanzibar ina fursa kubwa ya kujifunza kutokana na mafanikio yaliyopatikana katika Mahakama ya Tanzania katika matumizi ya Tehama, jambo litakalosaidia kuharakisha utoaji wa haki kwa wananchi na kupunguza gharama za kiutendaji. Aidha, Rais Dkt. Mwinyi ameusifu ushirikiano uliopo kati ya Mahakama ya Zanzibar na Mahakama Kuu ya Tanzania, akisisitiza umuhimu wa kuuendeleza ili kuongeza tija katika utekelezaji wa majukumu ya taasisi hizo. Ameeleza kuwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imeendelea kuwekeza katika matumizi ya Tehama pamoja na kuboresha miundombinu ya Mahakama katika ngazi mbalimbali ili kuhakikisha wananchi wanapata haki kwa haraka, kwa urahisi na katika mazingira bora yaliyo karibu na maeneo wanayoishi. Akizungumzia maendeleo ya miundombinu ya Mahakama, Rais Dkt. Mwinyi amesema ujenzi wa Mahakama ya Rufaa Pemba utasaidia kuimarisha mazingira ya kazi kwa majaji na kuongeza ufanisi katika utoaji wa haki kwa wananchi wa Pemba. Kwa upande wake, Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. George Masaju, ameipongeza Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Mahakama ya Zanzibar kwa ushirikiano wanaouonesha, huku akieleza kuwa uamuzi wa kuwa na Mahakama Kuu Pemba ni wa busara na wenye manufaa makubwa kwa wananchi. Ameahidi kusimamia kwa karibu utekelezaji wa mradi huo ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma za mahakama kwa urahisi zaidi na kwa gharama nafuu. #Zanzibar #Mahakama #Tehama #HakiKwaWote #DktMwinyi #GeorgeMasaju #UtawalaBora #AsamOnlineTV #Tanzania

KIMENUKA ZANZIBAR! ACT WAZALENDO YAPINGA KAULI ZA MAWAZIRI KUHUSU UZANZIBARI NA ZAN ID
▶︎

KIMENUKA ZANZIBAR! ACT WAZALENDO YAPINGA KAULI ZA MAWAZIRI KUHUSU UZANZIBARI NA ZAN ID

TISHIO LA MAANDAMANO 7/7, WAZIRI MKUU AFOKA VIKALI KWA WALIOPANGA MAANDAMANO ATOA MSIMAMO MKALI
▶︎

TISHIO LA MAANDAMANO 7/7, WAZIRI MKUU AFOKA VIKALI KWA WALIOPANGA MAANDAMANO ATOA MSIMAMO MKALI

CAG MSTAAFU PROFESA ASSAD AFUNGUKA SABABU ZILIZOPELEKEA KUONDOLEWA KATIKA NAFASI YA CAG
▶︎

CAG MSTAAFU PROFESA ASSAD AFUNGUKA SABABU ZILIZOPELEKEA KUONDOLEWA KATIKA NAFASI YA CAG

MASWALI MAGUMU ALIYOULIZWA WAZIRI MKUU MWIGULU BUNGENI - AYAJIBU kwa HOJA...
▶︎

MASWALI MAGUMU ALIYOULIZWA WAZIRI MKUU MWIGULU BUNGENI - AYAJIBU kwa HOJA...

Türkei – USA Highlights | Gruppe D, FIFA WM 2026 | sportstudio
▶︎

Türkei – USA Highlights | Gruppe D, FIFA WM 2026 | sportstudio

#BREAKING: WAZIRI KATAMBI APIGA STOP CCM - CHADEMA KUFANYA MIKUTANO - TISHIO LA MAANDAMANO SABASABA
▶︎

#BREAKING: WAZIRI KATAMBI APIGA STOP CCM - CHADEMA KUFANYA MIKUTANO - TISHIO LA MAANDAMANO SABASABA

Animals Being Ridiculous That Will Definitely Brighten Your Day 😂
▶︎

Animals Being Ridiculous That Will Definitely Brighten Your Day 😂

ACT WAZALENDO CONFRONTS KITWANA WITH TOUGH QUESTIONS ON THE UNION, "TALKING ABOUT ZANZIBARI IDENT...
▶︎

ACT WAZALENDO CONFRONTS KITWANA WITH TOUGH QUESTIONS ON THE UNION, "TALKING ABOUT ZANZIBARI IDENT...

Mikutano ya hadhara ya kisiasa Tanzania, yapigwa marufuku
▶︎

Mikutano ya hadhara ya kisiasa Tanzania, yapigwa marufuku

Rubio Reveals Israel-Lebanon Framework Peace Agreement: 'It's the Beginning of the Beginning'
▶︎

Rubio Reveals Israel-Lebanon Framework Peace Agreement: 'It's the Beginning of the Beginning'

BIBI wa SUMBAWANGA amvaa WAZIRI MKUU MWIGULU kwa madai haya MAZITO "sitaki kiwanja nataka hela"
▶︎

BIBI wa SUMBAWANGA amvaa WAZIRI MKUU MWIGULU kwa madai haya MAZITO "sitaki kiwanja nataka hela"

La Rocade prend forme : découverte des avancées impressionnantes du projet
▶︎

La Rocade prend forme : découverte des avancées impressionnantes du projet

Male lion attacks over 20 hyenas
▶︎

Male lion attacks over 20 hyenas

Heche Amshukia Patrobasi Katambi Kufungia Mikutano: 'Hauna Mamlaka Hayo'
▶︎

Heche Amshukia Patrobasi Katambi Kufungia Mikutano: 'Hauna Mamlaka Hayo'

“You’ll Never Be Like Us.” Until 500KG Happened 🔥
▶︎

“You’ll Never Be Like Us.” Until 500KG Happened 🔥

WANANCHI WAMGOMEA MKUU WA KITUO CHA POLISI DIWANI ACHARUKA MKUTANO WAVURUGIKA NA KUSAMBARATIKA
▶︎

WANANCHI WAMGOMEA MKUU WA KITUO CHA POLISI DIWANI ACHARUKA MKUTANO WAVURUGIKA NA KUSAMBARATIKA

Why Hydrofoil Boats Disappeared
▶︎

Why Hydrofoil Boats Disappeared

Israel, Lebanon sign framework deal with US, Marco Rubio calls it first step in 'difficult journey'
▶︎

Israel, Lebanon sign framework deal with US, Marco Rubio calls it first step in 'difficult journey'

Zanzibar Ministers must stop using the Union as an excuse for intimidation – ACT
▶︎

Zanzibar Ministers must stop using the Union as an excuse for intimidation – ACT

"DON'T THREATEN ME": HECHE RESPONDS TO MINISTER KATAMBI IN MPANDA, Reveals the Whole Story
▶︎

"DON'T THREATEN ME": HECHE RESPONDS TO MINISTER KATAMBI IN MPANDA, Reveals the Whole Story