LUMBERSA YATAJWA KUWA CHANZO CHA WAKULIMA KUPUNJWA MAPATO
Waziri Mkuu, wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba amesema mfumo wa uuzaji wa mazao usiotumia vipimo rasmi maarufu kama “Lumbesa” umekuwa moja ya njia inayochangia kuwaibia wakulima na wazalishaji wa mazao Nchini. Kutokana na hali hiyo, Dkt. Nchemba amewataka Watanzania kuachana kabisa na utamaduni wa kuaminiana katika biashara za mazao na badala yake kutumia vipimo rasmi na mifumo inayotambulika kisheria ili kuhakikisha wanapata thamani halisi ya mazao yao. Akizungumza Mei 19, 2026 katika kilele cha maadhimisho ya miaka 20 ya Bodi ya Stakabadhi za Ghala yaliyofanyika jijini Dodoma,Waziri Mkuu alisema Serikali imejipanga kikamilifu kukomesha matumizi ya mfumo huo usio rasmi ambao umekuwa ukiwakosesha wakulima haki zao. Aidha, ameuagiza Wakala wa Vipimo Nchini (WMA), Wizara ya Viwanda na Biashara, Wizara ya Kilimo pamoja na Ofisi ya Waziri Mkuu-TAMISEMI kushirikiana kwa karibu kuhakikisha mfumo wa Lumbesa unatokomezwa Nchini. “Tanzania haina uhaba wa vifungashio,ina viwanda vya kutosha vya kuzalisha vifungashio vya kutoshekeza mahitaji ya soko la bidhaa Nchini". Katika hatua nyingine, Serikali imetangaza kuanzisha mfumo wa malipo ya awali kwa wakulima wanaouza mazao yao kupitia mfumo wa Stakabadhi za Ghala, hatua inayolenga kuondoa changamoto ya wakulima kucheleweshewa fedha baada ya kupeleka mazao yao maghalani. Dkt. Nchemba alisema uamuzi huo umefikiwa baada ya Serikali kufanya majadiliano na wadau mbalimbali wa sekta binafsi, zikiwemo taasisi za kifedha pamoja na Benki ya Ushirika, kwa lengo la kuhakikisha wakulima hawapati tena adha ya kukopwa mazao yao bila malipo ya haraka. Amesema maboresho hayo yataongeza imani ya wakulima katika mfumo wa Stakabadhi za Ghala, kuongeza tija kwenye biashara ya mazao na kuchochea ukuaji wa uchumi wa wananchi na Taifa kwa ujumla. #DodomaFahariyaWatanzania #KeroyakoWajibuWanguTabasamunaSamia #KazinaUtuTunasongaMbele

Delivering The Plan: Voi - Taita Taveta Railway Line Coming Back to Life

በአፍሪካ ቀዳሚ ስንዴ አምራች ሀገር ኢትዮጵያ ሆናለች ETV | EBC | EBCDOTSTREAM

Uruhara rwa UPRONA mubwicanyi bwabaye muri 1972//Igitigiri c'Abahutu bishwe ku ntwaro ya MICOMBERO

MAELFU WAANDAMANA JERUSALEM NA TEL AVIV DHIDI YA NETANYAHU -VITA YA IRAN na LEBANON...

ጠቅላይ ሚኒስትር ዐቢይ አሕመድ (ዶ/ር) ስለዲጂታል ኢትዮጵያ 2030 የሰጡት ማብራሪያ | Pm Abiy Ahmed | Digital Ethiopia |

How I became Super Rich Without Ever being Employed!!MP Ndindi Nyoro!!

How US Air Force B 52 Pilot Performed an Emergency Takeoff at Full Speed

YALIYOJIRI DODOMA MEI 18 - 23, 2026

LIVE: UZINDUZI WA GHALA LA FORODHA LA CIWAYE

With These 20 New Mega Projects, Kenya is Overtaking All African Countries in 2026

Ibrahim Traoré : 5 000 km/an, le plan choc qui défie l’Occident au Sahel

MKURUGENZI MAJALIWA AFAFANUA KERO ILIYOWASILISHWA NA MWANANCHI KWA WAZIRI MKUU MWIGULU NCHEMBA

WATUMISHI WA UMMA WAMETAKIWA KUTOA HAKI KWA WANANCHI

Teacher and School Administrative Staff Transfer Calendar and requirements/criteria

SHERIA KATOLIKI ZA NDOA. Jifunze sheria muhimu za nsoa katika kanisa katoliki

MHE. SHAKA AWATAKA WAHE. MADIWANI KUTOJIHUSISHA NA MIGOGORO YA ARDHI KINYUME NA SHERIA.

SERIKALI KUJA NA MWAROBAINI WA CHANGAMOTO ZINAZOTOKANA NA MFUMO WA STAKABADHI ZA GHALA

YALIYOJIRI DODOMA MEI 11 - 16, 2026

RC Senyamule Asisitiza Matumizi ya Stakabadhi za Ghala Kulinda Maslahi ya Wakulima

