UWAJIBIKAJI NGUZO YA UTUMISHI BORA KWA WANANCHI: KIKWETE

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akizindua maadhimisho ya kitaifa ya wiki ya utumishi wa umma 2026 amewataka watumishi wa umma kutambua nafasi yao muhimu katika kuhakikisha huduma zinazotolewa zinakidhi matarajio ya wananchi. Maadhimisho haya yanayofanyika jijini Dodoma yamebeba kauli mbiu isemayo kuchochea uwajibikaji jumuishi, kwa huduma endelevu.