TULITUMIE JENGO HILI KULETA TAARIFA ZA RUSHWA - DG CHALAMILA

Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU Bw. Crispin Chalamila leo Juni 1, 2026 amezindua jengo la ofisi ya TAKUKURU mkoa wa Morogoro. Katika uzinduzi huo amemshukuru Raisi wa JMT Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuboresha mazingira ya utendaji kazi kwa watumishi wa TAKUKURU, huku akiwataka watumishi wa TAKUKURU kuyatunza na kuyathamini majengo hayo pamoja na vitendea kazi vilivyopo ili viweze kudumu kwa muda mrefu.