MIRADI MIKUBWA YA KIMKAKATI KUPITIWA NA MWENGE WA UHURU DODOMA
MIRADI MIKUBWA YA KIMKAKATI KUPITIWA NA MWENGE WA UHURU DODOMA Na Mwandishi Wetu, Dodoma RS Mkoa wa Dodoma umeupokea rasmi Mwenge wa Uhuru 2026 leo tarehe 31Mei 2026 katika Uwanja wa Shule ya Msingi Mtera, iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa, ukitokea Mkoa wa Iringa. Mwenge huo unatarajiwa kukimbizwa umbali wa kilomita 1,595.3 katika wilaya zote saba na Halmashauri nane za Mkoa huu, huku ukipita kuzindua, Kukagua,kuweka mawe ya msingi miradi ya maendeleo yenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 23.2 Akizungumza wakati wa mapokezi ya Mwenge huo, Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma, Dkt. Khatibu Kazungu, alisema Mkoa wa Dodoma umejipanga kuonyesha mafanikio makubwa ya utekelezaji wa miradi ya kimkakati inayotekelezwa kwa fedha zinazotolewa na Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan. Dkt. Kazungu alisema miradi hiyo imeendelea kuufungua Mkoa wa Dodoma kiuchumi, kuimarisha utoaji wa huduma za kijamii na kuufanya kuwa kitovu muhimu cha uwekezaji na utalii Nchini. “Tunamshukuru na kumpongeza Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuuletea Mkoa wa Dodoma fedha nyingi za maendeleo ambazo zimewezesha utekelezaji wa miradi mikubwa ya kimkakati yenye manufaa makubwa kwa Wananchi,” alisema Dkt. Kazungu. Aidha, alibainisha kuwa wananchi wa Mkoa wa Dodoma wameendelea kuenzi na kuzingatia ujumbe wa Mwenge wa Uhuru unaohimiza uzalendo, umoja, mshikamano na ushiriki wa Wananchi katika shughuli za maendeleo. Alisisitiza kuwa amani na umoja wa Kitaifa ni msingi muhimu wa maendeleo ya kiuchumi na kijamii, akieleza kuwa mazingira ya utulivu na mshikamano ndiyo yanayowezesha Taifa kuvutia uwekezaji na kufikia maendeleo endelevu. #DodomaFahariyaWatanzania #WekezaDodomaStawishaDodoma #KazinaUtuTunasongaMbele #MwengewaUhuru2026

Mbio za Mwenge wa Uhuru Mpwapwa 31.5.2026

LIVE: UZINDUZI WA GHALA LA FORODHA LA CIWAYE

Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma Awataka Wananchi Kujitokeza Kwa Wingi Kuupokea Mwenge wa Uhuru

Kondoa Mji Wakipokea Mwenge wa Uhuru

NO ESCAPE FOR RUTO: As Lsk Lawyers Moves To Court To Stop Rutos & Mbadi New Finance Bill 2026‼️

DAWA YA RUTO!! Listen to Gachagua Powerful remarks today in Bungoma Church destroying Kasongo badly!

UWANJA WA NDEGE WA KIMATAIFA WA MSALATO DODOMA KUANZA KUTUMIKA SEPTEMBA 2026

Kibano Kipya Wamiliki Apartment, Nyumba za Barabarani Dar:'Apartments Zimekuwa Genge la Kihalifu'

DAWA YA RUTO!! Watch how John Methu held Big Rally in Ol Kalou to campaign for DCP Candidate!

*MWENGE WA UHURU 2026 MKOA WA DODOMA KUPITA MIRADI YA BILIONI 23.2.

MATOKEO YA USAILI WA MAHOJIANO (ORAL) NA WALIOPO KWENYE KANZIDATA KUANZA KUWEKWA WAZI HIVI KARIBUNI

WANANCHI WA DABALO WAKITOA PONGEZI KWA RAIS DKT SAMIA

Sauti ya Mwananchi Kusikika: RC Awasha Mitambo!

Tunahesabu saa kuupokea Mwenge wa Uhuru Mkoa wa Dodoma. Shime Wanadodoma,tujitokezeke kwa wingi.

Ruto heart attack as Sifuna and his troop holds Mega Rally in Thika with 'Sisi Ndio Sifuna!'

RC Senyamule Asisitiza Matumizi ya Stakabadhi za Ghala Kulinda Maslahi ya Wakulima

RAIS DR SAMIA ATANGAZA KUPUNGUZA MATUMIZI YA MAFUTA SERIKALINI

MBIO ZA MWENGE 2026 - UFUNGUZI WA KITUO CHA POLISI TOANGOMA 2026.

MAADHIMISHO YA SAMIA DAY DODOMA YAFANA

