MBEGU INAYOTOA MAGUNIA 55 KWA HEKARI

Shirika la BRITEN limeratibu utoaji elimu ya kilimo kuhusu mbegu bora na mbolea kupitia shamba darasa la zao la mahindi kwa wakulima wa Mtaa wa Masigira Kata ya Tanga Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma.Elimu hiyo imetolewa ikiwa ni siku ya mkulima ambayo katika Manispaa ya Songea imefanyika katika kata ya Tanga ambapo kampuni mbalimbali za uzalishaji mbegu za mahindi zilitoa elimu ya ubora wa mbegu za mahindi na mbolea