Rais wa Benki ya Maendeleo Afrika (AfDB) atembelea Zanzibar
RAIS DK.MWINYI AKUTANA NA RAIS WA BENKI YA MAENDELEO YA AFRIKA Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi leo Jumamosi Februari 25, 2023 ameupokea ujumbe wa Benki ya Maendeleo ya Afrika-AfDB, ukiongozwa na Rais wake Dkt.Akinwumi Adesina Ikulu, Zanzibar. Rais Dk. Mwinyi ameishukuru Benki ya Maendeleo ya Afrika kwa kuunga mkono miradi mbalimbali ya Maendeleo Zanzibar ikiwemo ya kijamii katika sekta ya Afya , barabara, maji na sekta ya usafiri. Dk.Mwinyi alitumia fursa hiyo kuueleza ujumbe huo wa Benki ya Maendeleo juu ya hatua zinazoendelea na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kusimamia sekta zilizo chini ya uchumi wa buluu ambapo kwa upande wa utalii amewaeleza unachangia asilimia 30 ya pato la nchi. Naye, Rais huyo wa Benki ya Maendeleo ya Afrika Dk . Adesina alimuelezea mwenyeji wake Rais Dk. Mwinyi miradi ambayo Benki hiyo inasaidia zaidi ujenzi wa barabara na sekta nzima ya usafiri. Alisema kwa sasa Benki yake inasaidia ujenzi unaoendelea wa barabara ya Bububu-Mahonda-Mkototoni, ujenzi wa barabara Tunguu-Makunduchi na ya Mkoani- ChakeChake. Vilevile benki hiyo imejikita kusaidia ujenzi wa Uwanja wa ndege mpya wa Pemba na miradi kadha ikiwemo ya maji na ujenzi wa masoko pia tayari Benki ya Maendeleo ya Afrika imetenga dola za Kimarekani milioni 15 kuunga mkono sekta zilizochini ya Uchumi wa Buluu. 📅25 Februari 2023, 📍Ikulu , Zanzibar.

DKT. MWINYI ATANGAZA MAPINDUZI YA UCHUMI! ZANZIBAR YAFUNGUA MILANGO KWA WAWEKEZAJI DUNIANI

BAADA YA KUPOKEA NDEGE ZNZ RAIS MWINYI ATOA MAAGIZO KWA ATCL NDEGE ZIONGEZE SAFARI

ZANZIBAR YANG'AA, YAWEKA REKODI KIWANJA CHA NDEGE AFRIKA, NDEGE KUBWA KUINGIA

ACT: JKT si chombo cha Muungano, tunapinga vijana wa Zanzibar kulazimishwa kujiunga kisa ajira

CHEKI RAIS SAMIA ALIVYOSHIRIKI TAMASHA la VYAKULA vya BAHARINI (ZANZIBAR SEAFOOD FESTIVAL)...

RAIS MWINYI ASEMA HAYA KWA WALIOWEKEZA ZANZIBAR, FEDHA ZITAJENGEWA MIRADI HII

VIDEO: TAZAMA RAIS SAMIA AKIMUAGA RAIS NYUSI AIRPORT ZNZ, ULINZI UMETAWALA

RAIS MWINYI WA ZANZIBAR ALIVYOFIKA MSIBANI KWA HAYATI MWINYI BABA YAKE MZAZI

Hii hapa Siri ya Mafanikio ya Awamu ya 8

Sakho atinga Ikulu Zanzibar/ Rais Mwinyi ateta nae

🔴#LIVE: RAIS MWINYI ALIVYOSHUHUDIA UTIAJI SAINI KATIA YA SHIRIKA LA NDEGE LA ZANZIBAR na DUBAI..

Kiapo cha Maalim Seif kuwa makamu wa kwanza wa Rais Zanzibar

MELI YA KWANZA YA KIMATAIFA YASHUSHA MAFUTA ZANZIBAR

BENK YA DUNIA

DK.MWINYI ANGURUMAA KISIWA PANZA

RAIS SAMIA ALIVYOWASILI ZANZIBAR AKITOKEA OMAN, RAIS MWINYI, MAKAMU WA RAIS, WAZIRI MKUU WAMPOKEA..

OMO LEO ATEMA CHECHE KIEMBESAMAKI, AWEKA WAZI KINACHOELENDELA ZANZIBAR KWENYE SAKATA LA GNU

HILI NDO JENGO JIPYA LA UWANJA WA NDEGE WA KIMATAIFA WA ABEID AMANI KARUME ZANZIBAR - TERMINAL III

RAIS MWINYI NA MKE WAKE WALIVYOIPOKEA NDEGE MPYA BOEING 787 8 DREAMLINER.....

