LIFAHAMU KUNDI LA M23, SABABU ZA KUIVAMIA DRC

Kundi la waasi wa M23 wanaotajwa kufadhiliwa na Serikali ya Rwanda wanadaiwa kuuteka Mji wa Goma nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) baada ya mapigano yaliyodumu kwa wiki kadhaa dhidi ya vikosi vya jeshi la nchi hiyo (FARDC). Kwa mujibu wa tovuti ya The Guardian, eneo lililotawaliwa na mapigano hayo lenye majimbo ya Ituri, Kivu Kusini na Kivu Kaskazini yanaundwa na makundi ya zaidi ya 129, kundi kuu katika maeneo hayo ni kundi la waasi wa M23. Lifahamu kundi la M23 Kwa mujibu wa Tovuti ya The Guardian, ni vigumu kuzungumzia waasi wa M23 bila kutazama historia ya jamii ya Watutsi eneo la Mashariki mwa DRC, jamii hiyo pia inapatikana nchini Rwanda. Mwaka 2006 liliundwa kundi la National Congress for the Defence of the People (CNDP) lililoundwa na viongozi wa Watutsi waliopo Mashariki mwa DRC. Kundi hilo liliibuka kutokana na kuibuka mvutano wa kikabila kati ya Watutsi na makabila mengine, hasusan baada ya mauaji ya kimbari ya Rwanda mwaka 1994 na mgogoro wa wakimbizi nchini DRC. Kundi la waasi la RCD, ambalo lilikuwa limedhibiti eneo la Mashariki mwa DRC, lilikata tamaa kupata mwafaka wa kuingia kwenye maridhiano ya amani na Rais Joseph Kabila, wakihofia kupoteza ushawishi wao eneo hilo. Wakiongozwa na Laurent Nkunda, CNDP ililenga kuwalinda raia wa Kitutsi dhidi ya mashambulizi ya makundi ya wanamgambo wa Kihutu na kupata uwakilishi bora wa kisiasa kwa Watutsi katika Serikali ya DRC chini ya Rais Kabila. Kuundwa kwa CNDP kwa kiasi kikubwa kulitokana na kushindwa kwa mchakato wa amani na kutozingatiwa kwa mahitaji na usalama wa jamii ya Watutsi. Vita vya Kwanza na vya pili vya DRC kati ya mwaka 1996 hadi 2003 ziliingilia kati kisha mtandao tata wa ushirikiano wa kukabiliana na makundi hayo. Mtandao ulilenga kukabiliana na makundi ikiwemo Congress of the National Congress for the Defence of the People (CNDP) na M23 ambayo ni mrithi wa CNDP. Makundi hayo yanatuhumiwa kunufaika na mizozo ya ndani ya Serikali na biashara haramu ya madini kutoka migodi iliyopo mashariki mwa DRC. M23 ilianzia wapi? CNDP, kikiongozwa na Laurent Nkunda, awali kiliundwa ili kulinda jamii za Watutsi lakini lilijulikana kwa ukiukwaji wa haki za binadamu na biashara haramu. Mnamo 2009, makubaliano ya amani yalitaka kuunganisha vikosi vya CNDP katika jeshi la DRC, lakini mvutano uliendelea na kusababisha kuundwa kwa M23 mnamo 2012. Kundi hilo lilipewa jina baada ya makubaliano ya amani ya Machi 23, 2009 ambayo yaliahidi kuunganishwa kwa wapiganaji wa CNDP katika jeshi la DRC na kutambua mrengo wao wa kisiasa. Hata hivyo, kikundi cha CNDP kilidai kuwa makubaliano hayo hayakutekelezwa vyema na kuzaliwa kwa M23 ili kushinikiza madai yao. M23 inadai kulinda jamii za Watutsi na wanaozungumza Kinyarwanda nchini DRC, ikitaja vitisho kutoka kwa wanamgambo wa Kihutu na kushindwa kwa serikali kulinda usalama wao. Licha ya madai hayo, kundi hilo limekuwa likishutumiwa kwa ukiukaji mkubwa wa haki za binadamu, ikiwemo mashambulizi dhidi ya raia. Ripoti ya Umoja wa Mataifa inakadiria kuwa kufikia Januari 2025, kundi la M23 lilikuwa na wapiganaji kati ya 3,000 na 4,000. Hata hiyo UN imekuwa ikiishutumu Rwanda kwa kufadhili kundi hilo tuhuma ambazo Rwanda imekuwa ikikanusha kila mara. Balozi wa Rwanda katika Umoja wa Mataifa, Ernest Rwamucyo, jana alipokuwa akihutubia mkutano wa Baraza la Usalama la Afrika hakukanusha wala kuthibitisha madai hayo ya kuwa na mkono wao katika uvamizi huo wa M23. Aidha Rwanda imeendeleza madai kwamba kundi la wapiganaji la FDRL ambalo lilitajwa kuhusika katika vita vya kimbari vya 1994, lilikimbilia DRC na linatumiwa na taifa hilo kuendeleza muaji ya kimbari eneo la Mashariki mwa DRC, jambo ambalo Serikali ya DRC imekuwa ikikanusha. Waziri wa Mambo ya Nje wa Rwanda, Olivier Nduhungirehe aliieleza Associated Press (AP) kuwa uamuzi wa DRC kukatisha mahusiano yake na Rwanda ni kukiuka makubaliano ya kimataifa. “Kwa upande wetu tumechukua hatua stahiki kuwaondoa wanadiplomasia wetu nchini DRC ambao walikuwa hatarini kudhuriwa na vikosi vya usalama vya Congo,” amesema Nduhungirehe. Ripoti ya Umoja wa Mataifa mwaka 2022 iliangazia ushahidi wa Vikosi vya Ulinzi vya Rwanda kusaidia M23 na kuzidi kuzorotesha uhusiano kati ya Rwanda na DRC huku mzozo wa rasilimali ikiwemo madini ukitajwa kuwa sababu kuu ya vita hiyo. M23 wanavyojitanua M23 inaendelea kujitanua ndani ya DRC ambalo ni Taifa la nne kwa idadi kubwa ya watu barani Afrika, wanaokadiriwa kufika milioni 109 mwaka 2024. Mashambulizi ya M23 yaliyoanza wiki moja iliyopita nchini DRC yamebadilisha upepo wa hali ya usalama Mashariki mwa DRC.

Live: Algae turns Lincoln Memorial Reflecting Pool green in Washington, DC, after Trump renovations
▶︎

Live: Algae turns Lincoln Memorial Reflecting Pool green in Washington, DC, after Trump renovations

Nuclear Historian Reacts to Movies | Science vs Fiction
▶︎

Nuclear Historian Reacts to Movies | Science vs Fiction

CHAOS ERUPTS:Robert Mbui and Kimani Ichung'wah Clash Bitterly Over Finance Bill 2026 in parliament
▶︎

CHAOS ERUPTS:Robert Mbui and Kimani Ichung'wah Clash Bitterly Over Finance Bill 2026 in parliament

State sets restrictions after New World Screwworm cases found in other states
▶︎

State sets restrictions after New World Screwworm cases found in other states

Primary elections to watch Tuesday: Runoff races in Georgia & Alabama, DC mayoral race
▶︎

Primary elections to watch Tuesday: Runoff races in Georgia & Alabama, DC mayoral race

Only hours left to cast ballots in Georgia primary runoff races
▶︎

Only hours left to cast ballots in Georgia primary runoff races

DOJ charges 15 in Minnesota for opposing immigration enforcement
▶︎

DOJ charges 15 in Minnesota for opposing immigration enforcement

World awaits U.S.-Iran nuclear negotiations as some Strait of Hormuz traffic resumes
▶︎

World awaits U.S.-Iran nuclear negotiations as some Strait of Hormuz traffic resumes

Starmer bans social media, Farage activates Substack
▶︎

Starmer bans social media, Farage activates Substack

Georgia voters head to polls for primary runoffs including GOP Senate, governor
▶︎

Georgia voters head to polls for primary runoffs including GOP Senate, governor

Good Morning America Full Broadcast - Monday, June 15, 2026
▶︎

Good Morning America Full Broadcast - Monday, June 15, 2026

Good Morning America Full Broadcast - Tuesday, June 16, 2026
▶︎

Good Morning America Full Broadcast - Tuesday, June 16, 2026

2 Bay Area women die in Santa Cruz County beach tragedy
▶︎

2 Bay Area women die in Santa Cruz County beach tragedy

How to Keep Your Pets Safe from New World Screwworm
▶︎

How to Keep Your Pets Safe from New World Screwworm

Epstein Freakout? Watch MS NOW's analysis of NYT's new BOMBSHELL reporting
▶︎

Epstein Freakout? Watch MS NOW's analysis of NYT's new BOMBSHELL reporting

FBI Thwarts Terror Drone Attack on White House UFC Freedom 250 Event – 5 in Custody
▶︎

FBI Thwarts Terror Drone Attack on White House UFC Freedom 250 Event – 5 in Custody

U.S. expected to DESTROY Iran’s uranium stockpile
▶︎

U.S. expected to DESTROY Iran’s uranium stockpile

2 college students dead after being swept into ocean in California, family says
▶︎

2 college students dead after being swept into ocean in California, family says

2 Bay Area college students dead after being swept into ocean at Santa Cruz Co. beach
▶︎

2 Bay Area college students dead after being swept into ocean at Santa Cruz Co. beach