Ziara ya Mnadhimu Mkuu wa JWTZ Luteni Jenerali Salum Haji Othman kwa Walinda Amani Afrika ya Kati
ZIARA YA MNADHIMU MKUU WA JWTZ NCHINI CAR Mnadhimu Mkuu wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania Luteni Jenerali Salum Haji Othman amefanya ziara maalum katika Kikosi cha walinda amani kutoka Tanzania kinachohudumu nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati. Luteni Jenerali Salum Othman akiwa na ujumbe wake wamewasili katika uwanja wa ndege wa Berberati uliopo katika Mkoa wa Mambere Kadei na kupokelewa na Mwenyeji wake Kamanda Kikosi TANBAT 05 Luteni Kanali Adam Hamis Kiza, Maafisa na Askari mbalimbali wanaohudumu katika Ujumbe wa Umoja wa Mataifa, MINUSCA hapa Jamhuri ya Afrika ya kati. Luteni Jenerali Othman amepokelewa na gwaride la heshima lililoandaliwa na TANZBAT 5 na baadae kupokea taarifa ya utendaji kazi ya Kikosi Kutoka kwa Afisa Mkuu wa Operesheni Meja Amulike Kabale. Pamoja na mambo mengine Luteni Jenerali Salum Othman amepata wasaa wa kufanya mazungumzo na Kamanda Mkuu wa Vikosi vya Ulinzi wa Amani – MINUSCA Luteni Jenerali Sidiki Traole yanayolenga utendaji kazi wa Kikundi cha walinda amani wa Tanzania. Aidha, alipata fursa ya kufanya mazungumzo na maafisa na askari katika ukumbi wa Serengeti ambapo walinda amani hao walionesha ari, hamasa na utayari wa kutekeleza majukumu ya ulinzi wa amani huku wakifata sheria na taratibu za Umoja wa Mataifa, pamoja na za nchi husika. Katika ziara hiyo Luteni Jenerali Salum Othman ameambatana na Mwambata Jeshi wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa nchini marekani Brigedia Generali George Mwita Itang’are, Kanali Ally Juma Ally, Kanali AbdulAziz Rashid, Kanali Mustapha Mussa Hozza, Luteni Kanali Jofrey Clemence Kilyenyi, Meja Mariam Godian Tabaro na Kapteni Hemed Athumani Mwalim.

HISTORIA FUPI YA MEJA JENERAL ALFRED KAPINGA

HISTORIA YA KUSISIMUA YA HAYATI LUTENI JENERALI MWAKILINDILE TANGU AANZE JESHI MPAKA UMAUTI KUMKUTA

ZUMARI: MNADHIMU MKUU MSTAAFU WA JWTZ - ABULRAHMAN SHIMBO - 30/08/2021

Majenerali 16 JWTZ wastaafu, wataka nidhamu jeshini

WAZIRI WA ULINZI AONGOZA WAOMBOLEZAJI KUAGA MWILI WA MEJA JENERALI GIMONGE (MSTAAFU

Jenerali Mabeyo: Niliingia vitani nikiwa kijana mdogo | Ukichanja damu yangu imeandikwa JWTZ

MNADHIMU MKUU WA JWTZ LUTENI JENERALI SALUM OTHMAN AFURAHISHWA NA UJENZI WA NYUMBA 5000 MSOMERA

'SUPRISE' ya MKUU wa MAJESHI na WAZIRI wa ULINZI kwenye HARUSI ya MEJA JENERALI SIBUTI..

RAIS SAMIA ALIVYOWATUNUKU NISHANI YA MIAKA 60 MAKAMNDA JWTZ

Wanajeshi wa TANZBATT 5 wakabidhi jukumu la ulinzi wa amani wa UN kwa TANZBATT 6 nchini CAR

Mpambe wa Rais alivyowasilisha bahasha ya siri bungeni

Usiache kutazama JWTZ wafanya yao cheki hiii.....

MKUU WA MAJESHI APIGIWA SHANGWE BUNGENI, BARUA YAKE YA KUSTAAFU YATAJWA NA SPIKA

Makongoro Nyerere avunja mbavu , Amwambia KIKWETE wewe una NG'AA siogopi kustaafu, sasa hivi bado

Tunawashukuru sana walinda amani kutoka Tanzania, TANZBATT-08 : Watu wa jamii ya Mbuti, DR Congo

Inama ya Unity Club | Gen (Rtd) Fred Ibingira

MAGARI YA KIJESHI YAKUTISHA YENYE SILAHA NZITO ZAKIVITA YAKIPITA KATIKA MAADHIMISHO ZANZIBAR

JE UNAMJUA JENERALI MAYUNGA MTI MKAVU

IHERE IJISHO AKARASISI K'ABANA BATO | BATOJWE NA POLICE GUKORA AKARASISI

