MPANGO WA GUNDI ASILIA NA UBANI WAZINDULIWA ISIOLO
Gatuzi la Isiolo imekuwa mwenyeji wa uzinduzi wa Mpango Mkakati wa Chama cha Gundi Asilia na Ubani Kenya (GARA) wa miaka mitano kuanzia 2026 hadi 2030, unaolenga kuibadilisha sekta ya gundi asilia na ubani . Hafla hiyo iliandaliwa hapa isiolo na iliwaleta pamoja sekta na mashirika yakiwemo CRS ,maafisa kutoka Serikali ya Kitaifa, Taasisi ya Utafiti wa Misitu Kenya (KEFRI), Huduma ya Misitu Kenya (KFS), Millennium Water Alliance, wanachama wa GARA, washirika wa maendeleo pamoja na wadau kutoka magatuzi ya Isiolo, Samburu, Marsabit na Turkana. Akizungumza kwa niaba ya mkurugenzi wa taasisi ya KEFRI ,Dkt Musingo Tito mbuvi amesema kwa kuwa Isiolo ni mojawapo ya maeneo kame , taasisi hiyo hupeana miti ambayo hustahimili ukame . naye Dkt. Lawrence Mwongela ambaye ni waziri wa biashara na vyama vya ushirika gatuzi la Isiolo , akimwakilisha waziri wa maji ,mazingira na maliasili , alisema uzinduzi huo ni hatua muhimu katika kufungua fursa za kiuchumi zinazotokana na gundi asilia na ubani katika maeneo kame na nusu kame nchini. Aliongeza kuwa serikali ya gatuzi la Isiolo kwa ushirikiano na Shirika la Catholic Relief Services (CRS), Mpango wa maendeleo wa Merti (MID-P) pamoja na washirika wengine, inaendelea kutekeleza miradi ya kuboresha thamani wa gundi asilia na ubani kupitia kuongeza uzalishaji, kuimarisha biashara, kupanua masoko na kuhifadhi miti inayozalisha mazao hayo. Akimwakilisha Mkurugenzi wa Millennium Water Alliance nchini Kenya, mkurugenzi wa programu wa shirika hilo, Bi. June Samo Ngugi, alisema mpango mkakati wa GARA unatoa dira ya pamoja na mwongozo wa vitendo utakaosaidia kuifanya sekta ya gundi asilia na ubani kuwa yenye ushindani wa kimataifa. Kwa upande wake, Mjumbe wa Bodi ya GARA, Abdi Somo wa gatuzi la Isiolo, alisema eneo hili lina utajiri mkubwa ambao bado haujatumika ipasavyo katika uzalishaji wa gundi asilia na ubani. Alitaja mazao kama Gum Arabic, Hagar, Frankincense na Gum Tach kuwa yana thamani kubwa katika soko la ndani na kimataifa, lakini bado hayajatumika kikamilifu kutokana na changamoto mbalimbali katika mnyororo wa thamani. Mpango Mkakati wa GARA wa mwaka 2026–2030 unatarajiwa kuimarisha mnyororo wa thamani wa gundi asilia na ubani nchini kwa kuhimiza uzalishaji endelevu, kuboresha upatikanaji wa masoko, kuendeleza utafiti na ubunifu, pamoja Join this channel to get access to perks: / @wasotv WASO TV - Informing and Entertaining

The Trap Inside Kenya’s Education System | Drunken lectures

Decolonise Your Plate | A Walk Through Dr. Wanjiru’s Garden

The Most Important Country in Africa You’ve Never Heard Of (Djibouti 🇩🇯)

I left a life of luxury in America, only to come and live in isolation in Kenya | Tuko TV

MAANDALIZI YA UZINDUZI WA KICHINJIO CHA KISASA CHA ISIOLO YAPAMBA MOTO

1957 High School Debate. Nigeria, Ethiopia, Ghana & South Africa. Prejudice pt 1

ZAIDI YA MICHE 160,000 YAPANDWA ISIOLO KATIKA SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI
![[TIMELAPSE] 266 Days Fried Chicken & Ducks, Smoked Pork, Smoked Fish Go To Sell /Phương's Story](https://i.ytimg.com/vi/nYh0zD3gnA4/hqdefault.jpg?sqp=-oaymwEjCNACELwBSFryq4qpAxUIARUAAAAAGAElAADIQj0AgKJDeAE=&rs=AOn4CLBF9-Onf8kBygOu7wlY4ltOmEfbwQ)
[TIMELAPSE] 266 Days Fried Chicken & Ducks, Smoked Pork, Smoked Fish Go To Sell /Phương's Story

UNDER ATTACK!! Sifuna,Orengo forced to run for their safety after paid goons send to attack them

Governor Anyang Nyong'o, Kisumu County Commissioner on Sunday's Goon Attack

GAVANA GUYO AONGOZA MAADHIMISHO YA MADARAKA KATIKA ENEO LA MALKAGALA KAUNTI YA ISIOLO.

NSE Stock Updates: Equity Bank, ABSA, NCBA, Family Bank and Dividend Shares

JIDA MALIYU WE ARE ONE

ISIOLO YAANDAA MASHINDANO YA HUDUMA YA KWANZA KANDA YA MASHARIKI YA JUU

Only Pakistani Mechanics Can Repair This Giant Caterpillar Loader Tire

MUMINA BONAYA AHUTUBIA WAKAZI WA MALKAGALA WAKATI WA SHEREHE ZA MADARAKA DAY 2026, ISIOLO

Make Headlights Like Crystal Clear with Aluminum Foil-This Crazy Trick Actually Works!

MAADHIMISHO YA SIKUKUU YA MADARAKA YAFANYIKA MALKAGALA, ISIOLO

Kenya 3-1 South Africa HIGHLIGHTS | Junior Starlets Are Heading To The Morocco 2026 FIFA World Cup 🏆

