CP Hamduni: Mafunzo yaboreshe utendaji kazi, muonekano wa TAKUKURU

Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) amewataka watumishi wanaoshiriki mafunzo kutumia elimu na maarifa watakayopata kuboresha utendaji kazi, maadili na muonekano wa TAKUKURU. Mafunzo hayo yanayofanyika jijini Dodoma kati ya Februari 20 - 22, 2024 yamewakutanisha Maafisa wanaohusika na uelimishaji umma na mawasiliano kutoka vituo maalum, wilaya, mikoa na makao makuu ya TAKUKURU. #Rushwa#Mafunzo na Maadili#Rushwa ni Adui wa Haki