WAZEE YA PEMBA WAFUNGUKA MBELE YA MH OMO

Mkoa wa Kaskazini Pemba Mgombea urais wa Zanzibar kwa tiketi ya ACT Wazalendo Mhe. Othman Masoud Othman amesema kwamba mafanikio yoyote katika nchi yanahitaji kuwa na kiongozi muaminifu na waadilifu jambo litakaloleta heshima na mshikamano miongoni mwa wanaongozwa. Mhe. Othman ambaye pia ni mwenyekiti wa Taiafa wa chama hicho ameyasema huko Kambini Kichokochwe Jimbo la Kojani wilaya ya wete mkoa wa Kaskazini Pemba alipozungunza na wanachama na wananchi katika mkutano wa hadhara kuendelea na kampeni ya kuwania urais kwenye uchaguzi wa Oktoba mwaka huu. Mhe. Othman ambaye pia ni makamu wa kwanza wa Rais wa Zanzibar amesema kwamba Zanzibar sio nchi ya kuwa hivi ilivyo sasa kiuchumi na ilipaswa kuwa mbele zaidi, lakini kinachokwaza ni kukosekana kwa uongozi uliochaguliwa na wananchi na kwamba jeuri za viongozi walizonazo wanazowfanyia wananchi zinatokana na kutochaguliwa na wananchi wenyewe. Mgombea huyo amesema kwamba kauli ya uchaguzi wa mwaka huu ni wa kuinusuru Zanzibar ni jitihada za kuitoa katika balaa la viongozi wenye viburi wanaozulumu haki za wananchi na wanaotumia mbinu za ghiliba katika kuingia madarakani. Aidha amefahamisha kwamba kutokana dhuluma iliyopo , wazanzibari wengi wameshindwa kupewa hata vitambulivyo vya ukaazi jambo ambalo ni dhuluma kubwa na kwamba nilazima hali hiyo iondolewe ndio Zanzibar itaweza kukaasawa sawa na kurejeshwa mikononi mwa wananchi na kuondoa viburi walivyonavyo baadhi ya viongozi. Mhe. Othman amesema kwamba nchi ni ya wananchi wote na wao wanapaswa kuamua nchi yao eendeshwe naamna gani na kwamba uchaguzi ujao ni kuondoa kiburi cha viongozi kutowaheshimu wananchi na pia kuondoa ufusadi ndani ya Zanzibar. Amesema kwamba njia pekee inayohitajika ni kujitahidi kushirikiana kuwaondoa CCM na kupambana nao na kamwe wananchi hawapaswi kufanya mas-hara na nchi kwani wizi wao sio tu kwamba wanaiba kura ila wameiba nchi pia. Amewataka wananchi kuingia kifua mbele kwenye uchaguzi wakijua kwamba ACT ni washindi kwa kuwa wametumia nguvu, maarifa na ujana katika kuitumikia Zanzibar na kamwe wananchi hawatokubali kushindwa. Amefahamisha kwamba chama hicho kinakwenda kwenye uchaguzi sio tu kupiga kura bali pia kulinda ushindi wao kwa kuwa chama hicho tayari kimeonesha kupata ushindi kwa kuwa wananchi wamedhamiria kupata ushindi . Mgombea huyo amesema kwamba ni lazima kuirejesha nchi kwenye mstari na kwamba yapo mengi ambayo chama kimeyapanga kitakachoweka mustakabali mwema wa maendeleo ya Zanzibar. Amefahamisha kwamba viongozi wanaopewa uongozi kwa njia haramu ni hasara kubwa hasa kwa muislamu kula chumo la haramu na watoto wao huku muhusika akaondosha mazingatio ya kula haramu muda wote. Amesema kwamba mtazamo wa ACT hakuna sababu ya Zanzibar kuwa masikini kutokana na kuwepo sekta za lakini hivi sasa kazi hiyo halilipi kwa vile serikali haijajishughulisha kumuwezesha mvuvi kupata kipato kikubwa cha kazi hiyo. Amesema kwamba bahari ya Zanzibar inasamaki wakutosha hadi sasa na kamwe wavuvi hawajawafika kwa vile hakuna zana za kuvulia na wananchi wakafainidika na rasilimali yao hiyo. Amesema kwamba chama chake kikishinda watafuta teknolojia ya kweli na vyombo vya kweli ili wakavue kiukweli kwani Zanzibar inautajiri mkubwa sana lakini wananchi wanashindwa kwa kutowezeshwa. Amefahamisha kwamba hivi sasa wavuvi wa pweza wanakwenda kuuza kenya wakipata fedha hudhani wamepata nyingi ilighali ni robo tu thamani halisi ya bei ya soko wanayopata kwa vile hawajawezeshwa. Mgombea huyo pamoja na mambo mengine amesema kwamba tayari wamezungunza na kampuni ya kitaliana na kwamba wamekubali kuwawezesha wavuvi wa Zanzibar kuweza kuvua na kuuza kwa thamnai ya zaidi ya maratatu kwa bei ya sasa na kumudu kupambana na masikini. Akizungunzia zao la chumvi amesema kwamba hata wizara ilipo haijulikani lakini kinachotakiwa ni kuwawezesha wakulima wa zao hilo kuongeza thamani na kuongeza bei ya zao hilo Amefahamisha kwamba katika jitihada za kulikuza zao la chumvi wapo wataalamu wanaowafahamu na wameahidii iwapo watawezeshwa kuwepo kiwanda watanunua kwa bei nzuri chumvi yote itakayiozalishwa Zanzibar. Amefahamisha kwamba ni wajibu wa serikali kukuwezesha na kuongeza thamani ya mazao yanayozalishwa nchini ili uongeze tija na akawataka wananchi kuwaunga mkono ili kushirikiana nao katika kuongeza kipato cha wananchi na wakulima nchini baada ya ushindi wa uchaguzi Oktioba mwaka huu.

CCM Zanzibar hawauonei wivu Uzanzibari wao - Omar Said Shaaban | GUMZO MAALUM
▶︎

CCM Zanzibar hawauonei wivu Uzanzibari wao - Omar Said Shaaban | GUMZO MAALUM

"DON'T THREATEN ME": HECHE RESPONDS TO MINISTER KATAMBI IN MPANDA, Reveals the Whole Story
▶︎

"DON'T THREATEN ME": HECHE RESPONDS TO MINISTER KATAMBI IN MPANDA, Reveals the Whole Story

#LIVE🔴Mhe OTHMAN MASOUD AKIWAHUTUBIA WANACHAMA NA WANANCHI JIMBO LA #GANDO PEMBA  #OMO25 #JUSSA
▶︎

#LIVE🔴Mhe OTHMAN MASOUD AKIWAHUTUBIA WANACHAMA NA WANANCHI JIMBO LA #GANDO PEMBA #OMO25 #JUSSA

KIMENUKA ZANZIBAR! ACT WAZALENDO YAPINGA KAULI ZA MAWAZIRI KUHUSU UZANZIBARI NA ZAN ID
▶︎

KIMENUKA ZANZIBAR! ACT WAZALENDO YAPINGA KAULI ZA MAWAZIRI KUHUSU UZANZIBARI NA ZAN ID

HAFLA YA KUFUNGA MAFUNZO YA AWALI YA ASKARI WA ZIMAMOTO KOZI NAMBA 6/2026
▶︎

HAFLA YA KUFUNGA MAFUNZO YA AWALI YA ASKARI WA ZIMAMOTO KOZI NAMBA 6/2026

Mazungumzo na Mama Anna Tibaijuka: Oktoba 29 | Sakata la Yuda |Tanganyika-Zanzibar| Kesi Tundu Lissu
▶︎

Mazungumzo na Mama Anna Tibaijuka: Oktoba 29 | Sakata la Yuda |Tanganyika-Zanzibar| Kesi Tundu Lissu

OMO amwambia Samia: Usije ukatuuwa, hatujakukosea kitu | ZANZIBAR YAAMUA 2025
▶︎

OMO amwambia Samia: Usije ukatuuwa, hatujakukosea kitu | ZANZIBAR YAAMUA 2025

🔴 Duh: WAZIRI MKUU TAMKO ZITO ATOA | USALAMA WA NCHI, ACHIMBUA MAZITO
▶︎

🔴 Duh: WAZIRI MKUU TAMKO ZITO ATOA | USALAMA WA NCHI, ACHIMBUA MAZITO

CAG MSTAAFU PROFESA ASSAD AFUNGUKA SABABU ZILIZOPELEKEA KUONDOLEWA KATIKA NAFASI YA CAG
▶︎

CAG MSTAAFU PROFESA ASSAD AFUNGUKA SABABU ZILIZOPELEKEA KUONDOLEWA KATIKA NAFASI YA CAG

Kerr Fatou SO9 EP22 Ousainou & Amie Bojang Speaks Exclusively To Kerr Fatou
▶︎

Kerr Fatou SO9 EP22 Ousainou & Amie Bojang Speaks Exclusively To Kerr Fatou

AMSHITAKI MMEWE KWA WAZIRI MKUU "ANAJINYEA TU" Wananchi Wavunjika Mbavu
▶︎

AMSHITAKI MMEWE KWA WAZIRI MKUU "ANAJINYEA TU" Wananchi Wavunjika Mbavu

MZEE ALI ALILIA SHAMBA LAKE, OMO AMPA NENO LA MATUMAINI
▶︎

MZEE ALI ALILIA SHAMBA LAKE, OMO AMPA NENO LA MATUMAINI

SEREKALI RASMI YAFUNGA HOJA ZA MJADALA WA UBAGUZI ZILIZO IBUKA ZANZIBAR NA TANZANIA BARA
▶︎

SEREKALI RASMI YAFUNGA HOJA ZA MJADALA WA UBAGUZI ZILIZO IBUKA ZANZIBAR NA TANZANIA BARA

Hivi ndivyo OMO atakavyoifunguwa Pemba | KUELEKEA OKTOBA 2025
▶︎

Hivi ndivyo OMO atakavyoifunguwa Pemba | KUELEKEA OKTOBA 2025

MICHANGO YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI KUHUSU BAJETI YA WIZARA YA UJENZI NA UCHUKUZI 2026/2027
▶︎

MICHANGO YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI KUHUSU BAJETI YA WIZARA YA UJENZI NA UCHUKUZI 2026/2027

🔴#RECAP: OMO AIBUKIA  PEMBA TENA AWAPA SOMO  HILI JIMBO LA PUJINI KAMPENI ZA ACT WAZALENDO
▶︎

🔴#RECAP: OMO AIBUKIA PEMBA TENA AWAPA SOMO HILI JIMBO LA PUJINI KAMPENI ZA ACT WAZALENDO

TAZAMA TUKIO KUBWA LAIBUKA DKT. SAMIA AKIWA ANAWASILI, CHEKI  WALINZI WALICHOKIFANYA MBELE YA UMATI
▶︎

TAZAMA TUKIO KUBWA LAIBUKA DKT. SAMIA AKIWA ANAWASILI, CHEKI WALINZI WALICHOKIFANYA MBELE YA UMATI

SHUHUDIA UZURI WA KUVUTIA WA PEMBA
▶︎

SHUHUDIA UZURI WA KUVUTIA WA PEMBA

ITAKUSHANGAZA MAAJABU YA KIJIJI CHA JAMBIANI, HISTORIA VYAKULA, LUGHA
▶︎

ITAKUSHANGAZA MAAJABU YA KIJIJI CHA JAMBIANI, HISTORIA VYAKULA, LUGHA

ZIARA YA MKUU WA MKOA KUSINI PEMBA MH. MATTAR ZAHOR MASOUD KENGEJA KUSIKILIZA CHANGAMOTO ZA WANANCHI
▶︎

ZIARA YA MKUU WA MKOA KUSINI PEMBA MH. MATTAR ZAHOR MASOUD KENGEJA KUSIKILIZA CHANGAMOTO ZA WANANCHI