Salama Na KAJALA Ep 35 | JERAHA LA MOYO Part 1
#YAHStoneTown #SalamaNa #PodCast SUBSRIBE TO OUR CHANNEL https://bit.ly/YahStoneTownSubs Listen our Podcast on Spotify Link https://spoti.fi/2Uxr6Cm ApplePodcast Link https://apple.co/2Ou1bru GooglePodcast Link https://bit.ly/GooglePodcastSalamaNa Audiomack Link https://bit.ly/YahStoneTownAudioMack YouTube Link http://bit.ly/YoutubeSalamaNa Kajala Winfrida Masanja ndo jina lake alipopewa na Mama yake kipenzi alipozaliwa. Mama ambaye alikua akilitumikia jeshi la Polisi Tanzania miaka ya nyuma, ambaye alihakikisha binti yake huyu anakua katika maadili yaliyo bora na nidhamu yake iwe ya hali ya juu. So nini haswa kilitokea mpaka akawa si mtoto mzuri yule ambaye Mama alifanya kila aliwezalo kuhakikisha anakua hivyo miaka ya nyuma? Sasa ni Mama na mfanyabiashara anayejielewa tu. Ila yepi haswa ambayo yalishawahi kutokea kwenye maisha yake na ambayo hajivunii hata kidogo? Mimi na K tunafahamiana miaka mingi sana, mara ya kwanza tulikuna kwenye michezo, kwenye uwanja wa basketball wa Pazi pale Drive In enzi hizo, skuizi nadhani panaitwa Ubalozi maana ni mkabala kabisa na ubalozi wa Marekani na uwanja umo ndani ya nyumba za Tanesco na sisi pia tulikua tukipaita hivyo. I remember alikua anakuja kucheza na sisi enzi hizo yeye anasoma Jitegemee nami nasoma Makongo Secondary School, hakua mchezaji mkaaali ila alikua na juhudi, na kwa mujibu wa maongezi yetu haya aliniambia ile pia ilikua ni moja ya njia zake za kutoka nyumbani na kupata kijihewa ivi, kwa kukutana na watu tofauti 😀. Sisi tulikua tukimshangaa kwa mitkasi yake mingi, alikua anatoka, yuko na marafiki ambao walikua wakubwa kuliko yeye na kama alikua na mambo mengi ivi. Ila huko ndo kukua sasa, maana unachojifunza wakati unafanya jambo ndo hapo unapoweza kujua kama ni zuri au baya na kama lina faida nawe au laa. Next thing I know Kajala ni mpenzi wa producer mataaata haswa enzi hizo ndani ya P-Funk na kwenye story zetu za humu amezungumzia hilo kwa urefu haswa, vile walivyokutana, alivyokua anakaa nae, reaction ya wazazi wake na waalimu shuleni na mahusioano yao mpaka yalipofika tamati. Jinsi ambavyo walikua wakiishi yeye na PFunk bila ya Mama yake Majani kujua kama mwanae anaishi na mwanafunzi ndani ya nyumba yake na mpaka akapata mimba bila ya yeye kujua. Paula alipozaliwa ndo mambo yakawa hadharani. Mapenzi yake na PFunk yalikua na mambo mengi ambayo niliyauliza kwenye episode hii ya 35, walikutanaje, waliendeleaje, wazazi, Paula na pengine watu wengine kuhusika na mapenzi yao hayo. Aliniambia mwisho wa siku ilibidi afanye liwezekanalo ili aweze kutoka humo na maisha yaendelee na akafanikiwa kukutana na mtu mwengine Ila na kwake naye mambo hayakua matamu kama ambavyo yalianza. Yaliisha kwa machozi na chuki ambayo anadhani iko upande wa pili zaidi maana kwake maisha yamesogea na maombi yake ya kuanza upya yamebarikiwa. Kajala amepitia mambo mengi kwenye maisha yake ambayo mengine anajivunia na mengine siyo hata kidogo. Kama kawaida, yangu matumaini utaokota mawili matatu humu na ambayo pia kama nia na madhumuni yatakufanya ushangae na kujifunza mwisho wa siku. Tafadhali enjoy! Love, Salama. Soundtrack Yeah by @MarcoChali • Marco Chali Feat One The Incredible & Msam... Follow: Twitter: / yahstonetown Instagram: / yahstonetown Facebook: / yahstonetown

Salama Na KAJALA Ep 35 | JERAHA LA MOYO Part 2

Salama Na Lady Jaydee Ep 24 | POWERHOUSE Part 1

Ni mila gani uliyozaliwa nayo ambayo leo ungependa ibadilike? | Gumzo La Sato

This Dubai trip healed me in ways I can’t explain ✨

PLAYLIST - LULU MICHAEL NYIMBO 10 AMBAZO ZIPO KWENYE PLAYLIST.

Netwalking Show | Size 8 Breaks Down 💔 Why She Missed Her Mum's Burial After C-Section

Madam Rita Afunguka Asili Yake Na Alipozaliwa "Nina Makabila Matatu" | SALAMA NA MADAM RITA PT 1

Kenyan RNBs Love Songs ft Dj Freon Sauti Sol Elani Nyashinski Bensoul Nviiri Gilad Hart the Band

OBINNA SHOW LIVE: MAPENZI YA GHETTO | VJ Partelo & Diana

EXCLUSIVE: KAJALA: Natamani Paula aje ku-Date na Mtu Sahihi/Mume wangu alitaka nibaki jela/Iliniuma

Salama Na NANDY Ep 53 | MNOGESHAJI PART 1

Spend November With Me | Real Life, Real Vibes 💐

I have been out there working to ground my family, now I am living in isolation.

Confrontation - Par Bijou Ngoné et Big Taf - invite: Ndella Madior Diouf - Sam. 18 Juillet 2026

GIGY MONEY ALIA STUDIO, ADAI MASHA LOVE ANAMROGA AGOMBANE NA WATU, APOTEE!

Dr.Kambanda Ku Ingaruka Kagame Agiye Guhura nazo Zoa Kwinangira/Amarangamutima ye Muri Biro Politiki

Rock Bottom And Its Basement || Mkurugenzi Diastories 4 Ep 11

DJ NiiDO - Kenyan RNBs Love Songs Part 4 : Bien Njerae Mutoriah Kinoti Bensoul Charisma Okello Max

KAKA SUMMER NA MWAIPAYA WAKIWASHA BILA UOGA

