Dereva wa Kang'ata apigwa risasi baada ya wahuni kuvuruga mkutano

Dereva wa Gavana wa Murang’a Irungu Kang’ata alipigwa risasi kifuani leo baada ya wahuni kuvuruga mkutano wa Linda Mwananchi uliokuwa unaongozwa na Gavana wa Murang’a Irungu Kang’ata. Akizungumza baada ya kisa hicho, Kang’ata na viongozi wengine wa Linda Mwananchi walikashifu kisa hicho, wakitaka uchunguzi ufanywe na wahusika kukamatwa. Emmanuel Too anatukunjulia jamvi la Nipashe Wikendi kwa taarifa hiyo.