NYUMBA NI NYINGI DODOMA KARIBUNI WATANZANIA

Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya Azania Bw.Charles Itembe leo (11/06/2021) ametembelea mradi wa nyumba elfu moja (1,000) Iyumbu na Chamwino unaotekelezwa na Shirika la Nyumba la Taifa NHC akiwa na Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Benki hiyo Bw. Felix Maagi na kujionea ujenzi jinsi ujenzi unavyoendelea. Akizungumza mara baada ya kufika eneo la mradi na kujionea nyumba hizo Bw. Itembe amesema kuwa hatua iliyofikiwa ni dhahiri kuwa NHC imejipanga vyema katika kuhakikisha inakamilisha mradi huo kwa wakati kwa viwango na ubora wa hali ya juu. Shirika la Nyumba la Taifa linatekeleza mradi huo wa nyumba 1,000 kwa kupitia mkopo nafuu kutoka Benki ya Azania iliyoakasimiwa mamlaka na Benki Kuu ya Tanzania (BoT) na Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi.