WANANCHI WAPONGEZA MARIDHIANO YA CCM NA ACT WAZALENDO
Wananchi wa Zanzibar wamepongeza kusainiwa kwa Waraka wa Pamoja wa Maridhiano ya Kisiasa kati ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na ACT Wazalendo, wakieleza kuwa ni hatua muhimu itakayochangia kuimarisha amani, umoja na maendeleo ya Zanzibar. Wakizungumza katika maeneo mbalimbali ya Zanzibar, wananchi hao wamesema maridhiano hayo yameongeza matumaini ya kuimarika kwa mshikamano wa kisiasa na kuweka mazingira bora ya ushirikiano katika utekelezaji wa shughuli za maendeleo. Aidha, wamempongeza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar, Dkt. Hussein Ali Mwinyi, kwa kuonesha utayari wa kuendeleza mazungumzo yaliyowezesha kufikiwa kwa makubaliano hayo. Vilevile, wananchi hao wamempongeza Mwenyekiti wa ACT Wazalendo Taifa, Othman Masoud Othman, kwa kushiriki katika mchakato huo na kuweka mbele maslahi ya Zanzibar kuliko tofauti za kisiasa. Kwa mujibu wa wananchi hao, hatua ya viongozi hao wawili kufikia maridhiano ni ishara ya ukomavu wa kisiasa na dhamira ya dhati ya kudumisha amani, utulivu na mshikamano, ambayo ni msingi muhimu wa maendeleo ya kiuchumi na kijamii. Wananchi hao wamevitaka vyama vya siasa, viongozi na wananchi kwa ujumla kuunga mkono utekelezaji wa makubaliano yaliyofikiwa ili kuhakikisha maridhiano hayo yanadumu na kuendelea kuijenga Zanzibar yenye umoja, mshikamano na maendeleo endelevu. #Zanzibar #Maridhiano #CCM #ACTWazalendo #Amani #Umoja #Maendeleo #AsamOnlineTV #TrendingNow

SERIKALI KUIMARISHA SEKTA YA SHERIA NA HAKI ZANZIBAR; ZAIDI YA BILIONI 13.6 ZAWEKEZWA

LIVE🔴KINACHO ENDELEA MDA HUU KATIKA UKUMBI WA PICCADILY KOMBENI ZANZIBAR Mhe OTHMAN MASOUD ANA JAMBO

OMO ATOA DARASA MBELE YA RAIS MWINYI NA DKT SAMIA HII NI HISTORIA KWA UPINZANI

🔴#LIVE: MAJENERALI 17 JWTZ WAKIAGWA KIJESHI Baada ya Kustaafu Utumishi Jeshini

MSIBA MZITO KUTOKA ZANZIBAR

🔴#RECAP: OTHMAN MASOUD AFAFANUA SABABU ZA KUKUBALI MARIDHIYANO YA 2026 ZANZIBAR

Kwa nini ACT-Wazalendo wameungana na CCM kuunda serikali Zanzibar? Katika Dira ya Dunia TV.

WANACHAMA 200 WA CUF PEMBA WAHAMA CHAMA, WATAJA SABABU LUKIKI ZA UAMUZI HUO

DC SAID HAJI MRISHO AKAGUA KARO LINALOVUJISHA MAJI MACHAFU FORODHANI

RAIS SAMIA AWAJIBU JUMUIYA YA MADOLA SAKATA LA LISSU, "MATAMKO YANATUWEKA KATIKA WAKATI MGUMU"

WANANCHI WAPONGEZA MARIDHIANO YA CCM NA ACT WAZALENDO, WASEMA NI MSINGI WA AMANI NA MAENDELEO

Maridhiano Mapya Zanzibar: Je, Makubaliano ya CCM na ACT Wazalendo Yatadumu?

Kuingia ama Kutoingia SUK? | GUMZO LA MARIDHIANO 2026

DALILA ATELEKEZWA DAR AKIWA NA WATOTO 5 NA MTU ALIYEMTOA ZANZIBAR ILI KUMSAIDIA

ACT WAZALENDO BAADA YA MAKUBALIANO WAFUNGUKA

KOMREDI MBETO: KILIFANYIKA NI TAKWA LA KIKATIBA, MUDA SI MREFU TUTAPATA SERIKALI YA UMOJA WA KITAIFA

OTHMAN MASOUD AJILIPUA MBELE YA RAIS SAMIA ATOA TAMKO KWA TUNDU LISSU NA WAFUASI WAKE | KATIBA MPYA

Heated Debate on the Future of Reconciliation in Zanzibar | RECONCILIATION TALK

MSIKITI NA KANISA ZANZIBAR VYAFUNGWA

