BENK YA DUNIA

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ameishukuru Benki ya Dunia kwa misaada ya maendeleo inayoendelea kuipatia Zanzibar, inayochangia ukuaji wa uchumi na ustawi wa jamii. Rais Dkt. Mwinyi ameyasema hayo leo, 18 Mei 2026, alipokutana na Mwakilishi Mkaazi wa Benki hiyo nchini Tanzania, Bw. Nathan Belete, aliyefika Ikulu kuaga baada ya kumaliza muda wake wa kazi nchini pamoja na kumtambulisha Mkurugenzi Mpya anayechukua nafasi yake, Bw. Firas Raad. Ameeleza kuwa Zanzibar imepata mafanikio makubwa kutokana na misaada na ushirikiano wa muda mrefu na Benki ya Dunia katika nyanja mbalimbali za kiuchumi na maendeleo, na kumhakikishia mwakilishi huyo kuwa Zanzibar itaendelea kuimarisha uhusiano wake na Benki hiyo. Rais Dkt. Mwinyi amesema misaada ya Benki ya Dunia imeleta tija na mageuzi makubwa katika sekta ya elimu, afya na miundombinu nchini kwa kuimarisha rasilimali watu pamoja na kuzijengea uwezo wa kiutendaji taasisi mbalimbali. Akizungumzia sekta ya afya, amesema misaada hiyo imeiwezesha Zanzibar kuwa na mfumo madhubuti wa afya pamoja na kuwajengea uwezo watendaji wa sekta hiyo, kuimarisha upatikanaji wa vifaa tiba, na kuiomba Benki ya Dunia kuendelea kuweka mkazo zaidi katika kuongeza misaada ili kuwa na uwezo wa kudhibiti na kukabiliana na magonjwa mbalimbali. Akielezea Mradi wa Kuimarisha Miundombinu ya Barabara Mijini (BIG Z), amesema ameridhishwa na maendeleo ya mradi huo aliouelezea kuwa na umuhimu mkubwa kwa Zanzibar, na kuishauri Benki ya Dunia kuendelea kuuunga mkono ili kuleta mafanikio zaidi hatua kwa hatua. Aidha, ameishauri Benki hiyo kuendelea kuunga mkono juhudi za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kukabiliana na tatizo la uhaba wa umeme na kuhakikisha upatikanaji wa nishati ya uhakika. Dkt. Mwinyi amesema wakati umefika kwa Benki ya Dunia kuwa na afisi Zanzibar, kama ilivyofanyika kwa mashirika mengine ikiwemo Shirika la Afya Ulimwenguni (WHO) na Shirika la Kuhudumia Watoto la Umoja wa Mataifa (UNICEF), ambayo yote yana afisi zao Zanzibar. Rais Dkt. Mwinyi amemtakia heri Bw. Nathan Belete katika utekelezaji wa majukumu yake mapya. Naye Bw. Nathan Belete ameihakikishia Zanzibar ushirikiano zaidi katika utekelezaji wa miradi na mipango mbalimbali ya Benki ya Dunia, huku akisifu hatua kubwa za maendeleo katika sekta mbalimbali pamoja na usimamizi mzuri wa miradi inayofadhiliwa na Benki ya Dunia.

How Iran and the US went from friends to bitter foes - BBC Africa
▶︎

How Iran and the US went from friends to bitter foes - BBC Africa

UCHANGANUZI | Je Tanzania itarajie manufaa gani kupitia makubaliano ya Serikali na Singapore?
▶︎

UCHANGANUZI | Je Tanzania itarajie manufaa gani kupitia makubaliano ya Serikali na Singapore?

MTAFARUKU: Wazanzibari Wawachonokoa Watanganyika
▶︎

MTAFARUKU: Wazanzibari Wawachonokoa Watanganyika

#KUMEKUCHA: JAKU ACHAGA BARAZANI  ''sizungumzi kihindi '' ATAKA MAJIBU
▶︎

#KUMEKUCHA: JAKU ACHAGA BARAZANI ''sizungumzi kihindi '' ATAKA MAJIBU

Shakira, Burna Boy - Dai Dai (Official Video)
▶︎

Shakira, Burna Boy - Dai Dai (Official Video)

VIDEO: AGL YA WAFARANSA WALIOKABIDHIWA BANDARI YA ZANZIBAR, WAANZA KAZI RASMI NA VIFAA VYAO VYA KAZI
▶︎

VIDEO: AGL YA WAFARANSA WALIOKABIDHIWA BANDARI YA ZANZIBAR, WAANZA KAZI RASMI NA VIFAA VYAO VYA KAZI

Watalii zaidi ya 400 watua Zanzibar
▶︎

Watalii zaidi ya 400 watua Zanzibar

" ZANZIBAR ITAENDELEA KUJITANGAZA KAMA KITOVU CHA UWEKEZAJI NA BIASHARA ".....MHE. HEMED
▶︎

" ZANZIBAR ITAENDELEA KUJITANGAZA KAMA KITOVU CHA UWEKEZAJI NA BIASHARA ".....MHE. HEMED

Tanzania to Go Nuclear: President Samia Suluhu Hassan Confirms Talks with Rosatom | APT
▶︎

Tanzania to Go Nuclear: President Samia Suluhu Hassan Confirms Talks with Rosatom | APT

Why Sweden Is Becoming a Defense Powerhouse as Europe Rearms
▶︎

Why Sweden Is Becoming a Defense Powerhouse as Europe Rearms

RAIS WA ZANZIBAR, DK. MWINYI ALIVYOJIBU SWALI LA CHARLES WILLIAM KUTOKA WASAFI MEDIA
▶︎

RAIS WA ZANZIBAR, DK. MWINYI ALIVYOJIBU SWALI LA CHARLES WILLIAM KUTOKA WASAFI MEDIA

President Ruto wows Finland President as he Powerfully speaks during Kenya–Finland Business Forum
▶︎

President Ruto wows Finland President as he Powerfully speaks during Kenya–Finland Business Forum

Ethiopia’s Economy: Mamo Mihretu on Industrialisation, Growth and Economic Reform
▶︎

Ethiopia’s Economy: Mamo Mihretu on Industrialisation, Growth and Economic Reform

KENYA, TANZANIA, ETHIOPIA: THE BIDDING WAR FOR DANGOTE'S $17 BILLION REFINERY HAS BEGUN
▶︎

KENYA, TANZANIA, ETHIOPIA: THE BIDDING WAR FOR DANGOTE'S $17 BILLION REFINERY HAS BEGUN

Wolff Responds: "China and The U.S.: A Delicate Balance" Dated June 10, 2026
▶︎

Wolff Responds: "China and The U.S.: A Delicate Balance" Dated June 10, 2026

RAIS MWINYI NA  MWENYEKITI WA KAMPUNI KUZALISHA MWAMI
▶︎

RAIS MWINYI NA MWENYEKITI WA KAMPUNI KUZALISHA MWAMI

'Frustration': Trump keeps promising Iran deal and getting zero results
▶︎

'Frustration': Trump keeps promising Iran deal and getting zero results

Why Egypt is Terrified of Ethiopia’s Mega-Airport City!
▶︎

Why Egypt is Terrified of Ethiopia’s Mega-Airport City!

VIONGOZI WALIOAPISHWA  NA MHE RAIS
▶︎

VIONGOZI WALIOAPISHWA NA MHE RAIS

🔴 #ZBC LIVE : 20/11/2023 - JUMATATU - HAFLA YA KUWAAPISHA WAKUU WA MIKOA NA WAKUU WA WILAYA
▶︎

🔴 #ZBC LIVE : 20/11/2023 - JUMATATU - HAFLA YA KUWAAPISHA WAKUU WA MIKOA NA WAKUU WA WILAYA