MKUU WA JIMBO LA K/KATI AFUNGUA SEMINA YA KUJIKINGA NA MAJANGA KATA YA KAHE
Mkuu wa Jimbo la Kilimajaro Kati la KKKT Dayosisi ya Kaskazini, Mchungaji Javason Mrema, amefungua semina ya kujikinga dhidi ya majanga kwa Viongozi wa Serikali, wakulima na wafugaji wa Kata ya Kahe katika vijiji vya Oria, Ngasini na Mawala, akisisitiza umuhimu wa maandalizi ya mapema ili kupunguza madhara yanayosababishwa na majanga mbalimbali. Mradi huo wa kujenga jamii yenye ustahimilivu, kuimarisha maandalizi ya maafa, uhifadhi wa mazingira nauwezeshaji kiuchumi, unatekelezwa na Dayosisi tatu( Pare, Mwanga na Kaskazini) chini ya ufadhili kutoka Ujerumani kupitia KKKT Makao Makuu ambao unaratibiwa na KKKT Dayosisi ya Kaskazini Idara ya Uwakili inayoongozwa na Mchungaji Andrew Munisi ukiwa na lengo la kuijengea jamii uwezo wa kujianda, kukabiliana na kuendelea kuishi baada ya majanga. Akimkaribisha Mkuu wa Jimbo la kati, Mch. Munisi leo Juni 9, 2026 Uhuru Lutheran Hotel amesistiza umuhimu wa Sharika na jamii kujiandaa kikamilifu kukabiliana na majanga ya aina zote ya kibinadamu au ya asili ili kuepuka athari mbalimbali. Akizungumza wakati wa ufunguzi wa semina hiyo, Mch. Mrema aliongoza tafakari kutoka Mithali 22:3 inayosema, “Mwenye busara huiona hatari na kujificha; bali wajinga huendelea mbele wakaumia.” Alisema maandiko hayo yanawahimiza watu kuchukua tahadhari kabla ya majanga kutokea. Alibainisha kuwa katika miaka ya karibuni jamii imeendelea kushuhudia majanga mbalimbali yakiwemo mafuriko, ukame na matetemeko ya ardhi yaliyosababisha maafa makubwa, vifo, maumivu na kudhoofika kwa uchumi wa wananchi. “Mungu anataka watu wake wachukue tahadhari. Tunajifunza hilo kupitia simulizi la Farao aliyepata ndoto kuhusu njaa iliyokuwa inakuja, na Yusufu akaeleza namna ya kujiandaa mapema ili kuokoa maisha ya watu,” alisema. Mch. Mrema alisema wananchi wanapaswa kutumia maarifa waliyonayo kuhusu mazingira yao kuchukua hatua za kujikinga na madhara ya majanga, ikiwa ni pamoja na kujenga mifereji ya maji, kupanda miti na kuhifadhi mazingira. Aliwataka viongozi wa serikali za vijiji na vitongoji kuhamasisha wananchi kushiriki katika ukarabati wa mifereji na miundombinu mingine muhimu inayosaidia kudhibiti athari za mafuriko. Kwa mujibu wa Mch. Mrema, mafanikio ya kukabiliana na majanga yanategemea ushirikiano kati ya serikali, taasisi za dini na wananchi. Alisema wakati wa majanga hakuna mipaka ya dini wala itikadi za kisiasa kwani kila mmoja anapaswa kushiriki kuokoa maisha na mali za wananchi. “Taasisi za dini zimekuwa bega kwa bega na serikali katika kuwahudumia wananchi wakati wa majanga. Ushirikiano huu ni muhimu ili kupunguza madhara na kuwasaidia waathirika kurejea katika maisha yao ya kawaida,” alisema.

ASKOFU DKT. SHOO AFUNGUA SEMINA YA UWAKILI KWA WACHUNGAJI KKKT DAYOSISI YA KASKAZINI

Mazungumzo na Mama Anna Tibaijuka: Oktoba 29 | Sakata la Yuda |Tanganyika-Zanzibar| Kesi Tundu Lissu

ASKOFU SHOO AFUNGUA JUMA LA ASKOFU NA VIONGOZI WA VIJANA 2026, ATAKA WAJENGEWE UWEZO

CCM Zanzibar hawauonei wivu Uzanzibari wao - Omar Said Shaaban | GUMZO MAALUM

SEMINA YA KUJIKINGA NA MAJANGA KATA YA KAHE YAFANYIKA MCH. ANDREW MUNISI, WASHIRIKI WAUZUNGUMZIA

"DON'T THREATEN ME": HECHE RESPONDS TO MINISTER KATAMBI IN MPANDA, Reveals the Whole Story

How Proctor’s texts in Karen Read lawsuit could free dangerous criminals

What Happened to Pastor Pius Muiru?

KKKT-DAYOSISI YA KASKAZINI NI MFANO WA KUIGWA KWENYE UTUNZAJI WA MAZINGIRA - PROF. CYNTHIA LOBEDA

KIONGOZI MPYA WA VIJANA DAYOSISI YA KASKAZINI AINGIZWA KAZINI

TENZI ZA ROHONI - DEEP RELAX SWAHILI WORSHIP SONGS

Famous Biryani Street Food in Afghanistan | kabuli pulao | Roasted Chicken & Punjabi Curry | Rosh

OUTSIDER POLITIC #3. Constantin Toma: „Nu Grindeanu conduce PSD, ci familia Olguța - Claudiu”

COLLINS MUSHI ASTAAFU UONGOZI WA VIJANA KKKT DK

Afghan most Famous Kabuli Pulao | Pakistani Karahi | Biryani recipe | Roasted chicken | Street food

الرقية الشرعية للشفاءمن السحروالعين والحسد حصن من الشيطان رقية البيت والاولاد بصوت القارئ سعيد حمدان

HARAMBEE YA UJENZI WA NYUMBA YA IBADA KILIMA MOJA, MILIONI 127 ZAPATIKANA

PLO Lumumba BLASTS South Africa: "This Is Not Xenophobia, It's Afrophobia"

The FULL VIDEO of Trump they didn’t want released

