NAWEZAJE KUSHINDA DHAMBI.? Mwl.Bryan #revealjesus
Katika video hii nimeeleza kuhusu KUISHINDA DHAMBI. Nawezaje kuishinda Dhambi. Kwanza kabisa Lazima ujue nini kinasababisha dhambi.? .. jibu kwa ufupi ni Mwili utu wa kale ndio huketa Dhambi…Warumi 13:14 Bali mvaeni Bwana Yesu Kristo, wala msiuangalie mwili, hata kuwasha tamaa zake. Njia pekee ya kuufisha mwili ni kwa kumuamini Yesu na kujifunza kwake kumvaa kristo Warumi 8:12-13 12 Basi, kama ni hivyo, ndugu, tu wadeni, si wa mwili tuishi kwa kufuata mambo ya mwili, 13 kwa maana kama tukiishi kwa kufuata mambo ya mwili, mwataka kufa; bali kama mkiyafisha matendo ya mwili kwa Roho, mtaishi. Wagalatia 5:4, 16-21. Ili usizitimize Taama za Mwili yaktupasa kuto kuenenda kwa Mwili. 4 Mmetengwa na Kristo, ninyi mtakao kuhesabiwa haki kwa sheria; mmeanguka na kutoka katika hali ya neema. 16 Basi nasema, Enendeni kwa Roho, wala hamtazitimiza kamwe tamaa za mwili. 17 Kwa sababu mwili hutamani ukishindana na Roho, na Roho kushindana na mwili; kwa maana hizi zimepingana, hata hamwezi kufanya mnayotaka. 18 Lakini mkiongozwa na Roho, hampo chini ya sheria. 19 Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uchafu, ufisadi, 20 ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi, 21 husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu. Tena katika Waefeso 4:20-30 anazungumzua namna utu wakale na utu upya baada ya Kristo. 20 Bali ninyi, sivyo mlivyojifunza Kristo; 21 ikiwa mlimsikia mkafundishwa katika yeye, kama kweli ilivyo katika Yesu, 22 mvue kwa habari ya mwenendo wa kwanza utu wa zamani, unaoharibika kwa kuzifuata tamaa zenye kudanganya; 23 na mfanywe wapya katika roho ya nia zenu; 24 mkavae utu mpya, ulioumbwa kwa namna ya Mungu katika haki na utakatifu wa kweli. 25 Basi uvueni uongo, mkaseme kweli kila mtu na jirani yake; kwa maana tu viungo, kila mmoja kiungo cha wenzake. 26 Mwe na hasira, ila msitende dhambi; jua lisichwe na uchungu wenu bado haujawatoka; 27 wala msimpe Ibilisi nafasi. 28 Mwibaji asiibe tena; bali afadhali afanye juhudi, akitenda kazi iliyo nzuri kwa mikono yake mwenyewe, apate kuwa na kitu cha kumgawia mhitaji. 29 Neno lo lote lililo ovu lisitoke vinywani mwenu, bali lililo jema la kumfaa mwenye kuhitaji, ili liwape neema wanaosikia. 30 Wala msimhuzunishe yule Roho Mtakatifu wa Mungu; ambaye kwa yeye mlitiwa muhuri hata siku ya ukombozi. Imeandaliwa na Mwl. Bryan Frank #revelation #africa #revelation #april #pasaka #gospelmusic #sin #mafundisho #injili #neema #grace #jesus #yesu #yeshua #swahili #biblia

NITAMJUAJE MUHUBIRI WA UONGO.? Mwl.Bryan

Maana ya Jina lako katika ulimwengu wa Roho. Mwl.Bryan #identityinchrist #name

Mtoto Aliyepotea Njiani: Tumaini la Mungu kwa Waliotanga Mbali na Nyumbani | Lesson 12 | 17/06/2026

SIKU YA 3: YESU na UTAKASO WA WAKOMA KUMI (10). Mwl.Bryan #revealjesus

UNFORTUNATELY, WE HAVE TO RETURN TO AMERICA!!

HEKIMA NI NINI??

Je kuna vitabu ambavyo havipo kwenye Biblia.? Mwl.Bryan #revealjesus

There is no Normality for the Children of God. Mwl.Bryan #revealjesus

MAOMBI YA ASUBUHI. KUVUNJA KILA KIFUNGO By Pst Victor Tullo.

YEZEBELI MWANAMKE KATILI NA MCHAWI

Njia zako zikimpendeza Mungu tu unapata baraka na Utajiri udumuo.Mwl.Bryan #ibadahonline

SIKU YA 24: KAULI ya YESU IMEKWISHA. Yohana 19:28-30. Mwl.Bryan #revealjesus

UKIIJUA SIRI HII KUHUSU MIKOPO | HUTAKAA UKOPE | Pr.David Mmbaga |

Je UMEWAHI KUSOMA BIBLIA YOTE ⁉️. KARIBU MWAKA 2026 TUISOME. Mwl.Bryan #ibadahonline #biblia #2026

Best Hillsong Worship Songs 2026✝️ Morning Worship Playlist | Top Christian Praise & Worship Music

SIKU YA 19: je BADO FAHARI na VITU vya Duniani viko MKONONI Mwa SHETANi ⁉️. Bryan #revealjesus

UFUNUO, IDADI YA WATU WATAKAO INGIA MBINGUNI #heaven

🔴ሀጢአት መስራት አቁሙ! | STOP SINNING! - PROPHET TILAHUN TSEGAYE #jesus #protestantreformation #habesha

JINSI YA KUTEMBEA NA ROHO MTAKATIFU - PASTOR JOSEPH - EIC TV

