#TAZAMA| WAZIRI MKUU MAJALIWA AKERWA AMTUMBUA AFISA MIPANGO LIWALE
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amemsimamisha kazi Afisa Mipango wa Halmashauri ya Wilaya ya Liwale Bw. Omary Chingwile ili kupisha uchunguzi wa tuhuma za matumizi mabaya ya fedha za ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Liwale na kuviagiza vyombo vya ulinzi na usalama kufanya uchunguzi juu ya tuhuma hizo. “Hatuwezi kufanya mchezo na fedha ya Serikali. Tunahitaji kila mradi uende vizuri, fedha iliyoletwa lazima itumike kama ilivyokusudiwa.” Mheshimiwa Majaliwa amesema Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza matumizi mazuri ya fedha za umma ili zikamilishe miradi ya maendeleo ya wananchi na kwamba Serikali haitamvumilia mtumishi yoyote anayetumia vibaya fedha za umma. Waziri Mkuu amemsimamisha kazi mtumishi huyo jana (Alhamisi Oktoba 7, 2021) wakati akizungumza na madiwani, watumishi na wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Liwale akiwa katika ziara ya kikazi ya kukagua miradi ya maendeleo katika Mkoa wa Lindi. Pia, Waziri Mkuu amelitaka Balaza la madiwani wa Halmashauri ya wilaya ya Liwale lisimamie vyema fedha za miradi zinazotolewa katika Halmashauri hiyo ikiwa ni pamoja na kubuni vyanzo vipya vya mapato. “Waheshimiwa madiwani, Halmashauri yenu inakusanya mapato hadi asilimia 100 lakini hatujawahi kuona mradi wowote unaotekelezwa na halmashauri na ukawa wa mfano.” Alisema Halmashauri hiyo imekuwa ikiweka makadirio madogo ya makusanyo ili ionekane inakusanya kwa asilimia kubwa lakini hata mapato yanayokusanywa, hayakusanywi kwa njia za kielektroniki na kumuagiza Mweka Hazina wa Halmashauri hiyo Gervas Bidogo kuhakikisha vifaa vyote vya kukusanyia fedha kwa njia ya kielektroniki (POS) vinafanya kazi. Follow us on: FACEBOOK; SpotiLeo: / spotileo-176. . HabariLeo: / habarileo DailyNews: / dailynewstz INSTAGRAM; HabariLeo: https://instagram.com/habarileo_tz?ig... SpotiLeo: https://instagram.com/spotileo?igshid... TWITTER; Twitter HabariLeo: https://twitter.com/HabariLeo?s=09

WAZIRI MKUU MAJALIWA AMSIMAMISHA KAZI MKURUGENZI na MWEKA HAZINA, WAJICHANGANYA FEDHA za SERIKALI

HECHE AMEKIWASHA UPYA AFICHUA KESI YAO AMJIBU KENANI BILA UOGA, HATUWEKWI MFUKONI SISI

UWEKEZAJI WA MIZENGO PINDA DODOMA NI BALAA EBU SHUHUDIA ALICHOKIFANYA

UTAPENDA! WAZIRI MKUU Alivyomuita MKE WAKE Jukwaani - "MAMA MAJALIWA NJOO"

Waziri Mkuu katoa saa 72, kwa Mkurugenzi na Mweka Hazina wa Halmashauri ya Ukerewe.

WAZIRI MKUU ANAZUNGUMZA NA WANANCHI WA KATA YA MGONGO,IRAMBA

WAZIRI MKUU MAJALIWA AKASIRIKA - AMTUMBUA INJINIA PAPOHAPO - AAGIZA MKURUGENZI ALIYESTAAFU AITWE...

🔴#TBCLIVE: ZIARA YA KIKAZI YA WAZIRI MKUU MKOANI MWANZA

HALMASHAURI YA MJI HANDENI KUTOA 50,000 KWA ATAKAEFICHUA BODABODA MWENYE MAHUSIANO NA WANAFUNZi

"Haiwezekani, Simamisheni Ujenzi, Mkandarasi na Mshauri Wanione Haraka"- WAZIRI JAFFO

Waziri Mkuu Majaliwa aagiza milango yote ibadilishwe Hospitali ya Wilaya ya Namtumbo. – Ruvuma.

MAJALIWA ATOA NENO KIFO CHA KIONGOZI CCM

WAZIRI MKUU AKUMBANA NA MKASA MZITO NYAMAGANA MWANZA,DAKTARI MWINGINE AMDHALILISHA MGONJWA.

🔴 #LIVE :Full package ziara ya kushtukiza ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Tanesco

WAZIRI MKUU ALIVYOMBANA MKUU WA IDARA YA MANUNUZI MKURANGA, BIL 2.6 ZATUMIWA VIBAYA

🔴#LIVE: WAZIRI MKUU ANAZUNGUMZA MUDA HUU CHEMBA -DODOMA

WAZIRI MKUU AMTUMBUA MKANDARASI "HAIWEZEKANI, ONDOA KUBEMBELEZA SIO SERIKALI HII"

🔴LIVE: HAFLA YA UTIAJI SAINI NA UZINDUZI WA MIRADI YA NISHATI SAFI

🔴 MUBASHARA: BAJETI KUU 2026/2027 INAWASILISHWA BUNGENI LEO

