Waziri Magufuli achukua fomu kuomba Kuteuliwa Kugombea Urais kupitia CCM
Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli alisaini kitabu kabla ya kuchukua fomu ya kuomba kuteuliwa kugombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi CCM mkoani Dodoma. Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa (Nec) ya Idara ya Oganizesheni, Dk. Mohamed Seif Khatibu ndiye aliyemkabidhi fomu Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli. Safari ya chama cha mapinduzi ya kupata mgombea wa urais katika uchaguzi mkuu ujao imeendelea kushika kasi baada ya makada sita wa chama hicho kuchukua fomu hii leo tarehe 04.06.2015 na kufanya jumla ya makada 11 wa chama hicho kujitokeza ndani ya siku mbili tangu zoezi hilo lifunguliwe rasmi june tatu mwaka huu. Miongoni mwa waliojitokeza kuchukua fomu hii leo ni pamoja na waziri mkuu mstaafu awamu ya tisa Mhe Edward Lowassa mbunge wa jimbo la Monduli ambaye amejinadi kuwa hana mpango wa kushindwa na amechoka na siasa za matusi na tuhuma na kudai kuwa hiyo sio demokrasia kwa viongozi wenye nia ya kweli ya kulikomboa taifa. Mwingine ni aliyewahi kuwa waziri mkuu wa awamu ya nane Fredrick Sumaye ambaye amebainisha kuwa endapo atapata ridhaa ya chama hicho ya kuwania urais na kushinda atahakikisha anatokomeza kabisa tatizo sugu la rushwa kwa kuunda vyombo maalum ikiwemo mahakama ya wala rushwa huku akitumia rasilimali za asili zilizoko nchini kuinua uchumi wa watanzania. Kada mwingine aliyejitokeza ni John Pombe Magufuli ambaye hivi sasa ni waziri wa ujenzi lakini pia amewahi kushika nyadhifa mbalimbali serikalini na ndani ya CCM kwa ufanisi wa hali ya juu ambaye yeye ametamba kipaumbele chake cha kwanza ni kutekeleza kwa vitendo ilani ya chama cha mapinduzi. Makada wengine waliojitokeza ni makamu wa rais Dk Mohamed Gharib Bilal, balozi Ali Karume na mwanafunzi wa chuo kikuu cha Mzumbe Morogoro Amos Siyatenzi huku makada wengine zaidi wakitarajiwa kujitokeza katika muda ambao chama hicho kimeweka kuanzia june 3 mpaka jully 2.

Magufuli Akishukuru chama Kumteua Kugombea Nafasi Ya Urais.

Rais Magufuli tena kuhusu sakata la dawa za kulevya, agizo jipya kuhusu Watanzania waliofungwa nje

LOWASSA AJIUZULU UWAZIRI MKUU

NCHIMBI ASOMA MESEJI ALIYOTUMIWA NA HAYATI MAGUFULI HADHARANI "SIWEZI KUHARIBU FUTURE YAKO"

Lowassa bungeni1 3

MAGUFULI - "NILINYWESHWA SUMU, KIKWETE ALINIFUKUZA, SIKUKATA TAMAA"

Rais Magufuli ametaja mshahara wake leo

Kikwete Ampa Tano Magufuli

Walininywesha Sumu, Nilitaka Kujiuzulu...Magufuli asimulia, almanusura imtoe uhai wake

Umunsi mbona Afande (Perezida Kagame) ni bwo nemeye ko mfite amahoro- DCG Ujeneza wahoze muri EX-FAR

Taarifa ya Uteuzi wa Mgombea wa urais CCM.

Chozi la Mkurugenzi baada ya Mbunge wa Chadema kumchongea kwa JPM

TOP 10: KAULI za JPM ZILIZOTIKISA, TAZAMA UNIAMBIE IPI ILIKUKOSHA ZAIDI!

KAPTENI KOMBA ALIVYOFARIKI KABLA YA 'URAIS WA LOWASSA, ALIFUTA JINA LA KIKWETE AKAWEKA LA MKAPA 1995

Magufuli aamsha dude jingine bandarini

“Nina hasira, Mimi nina uchungu na nchi yangu” –Ruge Mutahaba

HUYU NI MHE JOHN POMBE MAGUFULI 14 Nov 2013

makabidhiano ya ofisi kati ya Rais Magufuli na JK Novemba 12,2015

HD: RAIS MAGUFULI AWAFOKEA WACHINA "NI UPUMBAVU, HAMJAVAA BARAKOA MNACHELEWESHA MKATWE HELA"

