UTEKELEZAJI WA MITAALA ILIYOBORESHWA – SEKONDARI YA UFUNDI IFUNDA - IRINGA
IRINGA Mnamo tarehe 09 Disemba 2023, Serikali kupitia Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia ilitoa waraka wa Elimu namba 5, Waraka huu ulihusu utekelezaji wa mitaala iliyoboreshwa. Leo Tupo hapa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa, kupitia ofisi ya uthibiti ubora wa shule katika Halmashauri hii, tumeweza kuandaa Makala hii inayoonyesha matokeo chanya ya utekelezaji wa maboresho. Shule ya Sekondari ya Ufundi ya Ifunda, ni miongoni mwa shule inayotekeleza mkondo wa amali Kwa mujibu wa Mkuu wa shule Bwana Amani Jeremia Nyahi waalimu ambao wameajiriwa katika shule hii ni 59. Ofisi ya Uthibiti wa Ubora wa shule ni wakala Mkuu wa Serikali katika utekelezaji wa mabadiliko haya Utekelezaji wa mitaala iliyoboreshwa unafanyika kama ifuatavyo:Kwa Elimu ya Awali na Msingi, utekelezaji ulianza mwezi Januari, 2024 kwa shule zote nchini kwa Madarasa ya Elimu ya Awali, Darasa la Kwanza na Darasa la Tatu. Kwa upande wa shule za Sekondari ya Chini, utekelezaji wa Mkondo wa Amali pia ulianza Januari, 2024 katika baadhi ya Shule za Serikali na zisizokuwa za Serikali zilizothibitika kuwa na mahitaji muhimu ili kuleta ufanisi katika ufundishaji na ujifunzaji huku zoezi la uchaguzi wa Mikondo stahiki ukifanyika kwa ufanisi Maeneo yaliyoboreshwa ni pamoja na Muundo wa Elimu, Mikondo ya Elimu ya Sekondari, Moja ya masomo mapya ni Historia yaTanzania na Maadili somo litakalofundishwa katika ngazi zote za elimu kwa Lugha ya Kiswahili ikiwa ni pamoja na shule zinazotumia Mitaala ya Kimataifa somo hili limebeba maudhui yanayolenga kujenga Mtanzania mwenye uzalendo na uwajibikaji anayefahamu na kuzingatia historia, desturi, miiko na maadili ya nchi yake. Lugha ya Kufundishia nayo ni miongoni mwa maboresho Aidha, kwa wanafunzi wenye mahitaji maalumu ya ujifunzaji, Lugha ya Alama, Maandishi ya Breille na Lugha ya Alama Mguso zitatumika katika ufundishaji na ujifunzaji kulingana na mahitaji ya ujifunzaji ya mwanafunzi husika Mapitio ya Sera na maboresho ya mitaala yanalenga kuwa na wahitimu wenye maarifa, mwelekeo, rnaadili na ujuzi unaoakisi mahitaji halisi katika taifa letu na kuweza kushindana na kushiriki kikamilifu katika soko la ajira duniani. Pia, yamezingatia masuala muhimu yanayopewa kipaumbele katika dunia. Masuala hayo ni pamoja na mabadiliko ya tabianchi, elimu kuhusu Uraia wa Dunia (Global Citizenship Education) na Stadi za Karne ya 21. MWISHO Tukuswiga Mwaisumbe –Makutano TV

TV ART SLIDESHOW 24/7 | Vintage Floral Gallery 🌼4K Framed Art Screensaver for Living Room

WE ARE CHAMPIONS - IFUNDA TECHNICAL SECONDARY SCHOOL

JANITOR vs THE BIGGEST GUYS IN THE GYM. They Didn’t Expect THAT

MWANAFUNZI ASIYEONA AIBEBA NYANDA ZA JUU KUSINI TUZO ZA BMT 2026

"WAZIRI AMEONGEA KITU AMBACHO HAKIJUI" MADELEKA AMPASUA KATAMBI BILA UOGA

Siwa Kikala of Kombolela (Amina Vicoba) cracks everyone up, reveals she’s marrying a Mpemba this ...

The MAN who changed FOOTBALL forever | Pelé | Documentary

TRAINING IN 104 DEGREES! ☀️ | Day in Life of a Cyborg #44 | Arda Saatci

LUPASO SEC SCHOOL ICT LAB DOCUMENTARY

Africa Suffering Because We Elect The 'Worst' To Lead Us – Lumumba

Ethiopia is About to Explode.

The hidden treasures of Sudan - Heart of Africa - Travel documentary - AMP

Powering Possibilities: How Trust Transformed Communities Across Tanzania

A Side of Jamaica The Media Won't Show You!

Saxony-Anhalt: Why this election will be a fateful day for Germany | NIUS Live

Epic Congolese Wedding Dance Choreography - Battle Girls vs Boys None stop Entertainment /Australia

MKE NA MAHARI / NANI ALIPE MAHARI MZAZI AU KIJANA?

WATOTO ZAIDI YA 300 NZIHI WAHITAJI MABORESHO UPATIKANAJI HUDYMA YA MALEZI MCHANA

Qui sont les vrais ancêtres des Haïtiens ?

