TANZANIA MWENYEJI MKUTANO WA 6 WA USALAMA WA ANGA AFRIKA MASHARIKI
Mkutano wa sita wa Taasisi inayosimamia Ulinzi na Usalama wa Usafiri wa Anga Afrika Mashariki (CASSOA) unatarajia kufanyika kuanzia tarehe 15 hadi 16 Mei 2024 , katika Hoteli ya Verde visiwani Zanzibar. Mkutano huo utawakutanisha wadau muhimu wa Usafiri wa Anga ikiwa ni pamoja na makampuni ya ndege, viwanja vya ndege, wasimamizi na wadau wa usalama katika sekta ya anga kutoka nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki ambapo pia wajumbe watajadili maswala ya utunzaji wa mazingira. Akizungumza na waandishi wa habari Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) Hamza Johari amesema mikutano ya EAC Aviation ilianzishwa na Bodi ya EAC-CASSOA kama njia ya kuongeza uelewa juu ya maswala yanayoathiri Usalama wa Usafiri wa Anga katika kanda yetu wa Africa Mashariki na Duniani kwa ujumla. Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania ni taasisi ya umma yenye jukumu la kudhibiti sekta ya usafiri wa anga katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mamlaka iliundwa kwa Sheria ya Usafiri wa Anga, Sura ya 80 (R.E 2006). Majukumu ya kisheria ya Mamlaka ni kudhibiti masuala ya ki-usalama, ki-uchumi katika usafiri wa anga na kutoa huduma za uongozaji ndege. Pia Mamlaka inatoa huduma za uongozaji ndege kwenye vituo vya ndege kumi na nne (14) ambavyo ni: Dar es Salaam, Kilimanjaro,Tanga, Arusha, Mwanza,Tabora,Kigoma, Dodoma, Iringa, Songwe, Songea, Mtwara, Zanzibar na Pemba

Mahojiano Radio 5 Kuhusu Haki za Msafiri na Mtumiaji wa Usafiri wa Anga

KAMATI YA KUDUMU BUNGE YA MIUNDOMBINU YATEMEBELEA MRADI WA UJENZI CATC

SGR TABORA KIGOMA UJENZI UNASONGA MBELE

Mkurugenzi Mkuu TCAA Ndg.Hamza Johari Akizungumza Katika Kipindi Cha Tunatekeleza TBC ONE

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu Yafanya Ziara ya Kikazi TCAA

🇧🇫60 Massive Projects Transforming Burkina Faso

KAMATI YA KUDUMU BUNGE YA MIUNDOMBINU YATEMEBELEA MRADI WA UJENZI CATC

Inside Ethiopian Airlines: The A350-1000 Flight Operation

PROF.MBARAWA ARIDHISHWA NA MRADI WA UJENZI WA CATC, ASISITIZA UBORA NA KUAKISI THAMANI YA FEDHA

SAFARI YA MIKUMI

China Is Building East Africa's Largest Port in Tanzania

Fatou Bensouda on Israeli threats against her and the ICC | Talk to Al Jazeera

I Visited The North Korea of Africa!(Eritrea)!

Inside UN Aviation: IL-76 Humanitarian Airdrop Mission

| MONDAY REPORT | LAW OF IMPEACHMENT | CHARLES KANJAMA |

TIKETI YAKO HAKI YAKO - MWANZA

42ND ORDINARY LICENSING BOARD MEETING ON AIR AND GROUND HANDLING SERVICES

After Years of Delays, Kenya’s Refinery Gets a Launch Date

RIGATHI IMEACHED!!SHOCKED RIGATHI AFTER COURT CONFIRMED IMPEACHED AS FIRST DEPUTY PRESIDENT OF KENYA

