Dada Grace Omollo || Ushuhuda

Kwa hakika, kazi ya Yesu msalabani hutimia pale mtu aasipo dhambi, kumtwika Yesu mizigo yote mizito na kuchukua nira yake Yesu iliyo nyepesi na laini. Paulo asema, katika Waefeso 5:8-12 " Zamani ninyi pia mlikuwa gizani, lakini sasa mmekuwa nuru katika Bwana; basi muishi kama watoto wa nuru. 9 Kwa maana tunda la nuru hupatikana katika kila lililo jema, lililo la haki na la kweli. 10 Jifunzeni mambo yanayom pendeza Bwana. 11 Msishiriki matendo ya giza yasiyofa a, bali yafichueni. 12 Kwa maana ni aibu hata kutaja mambo wanayofanya kwa siri." Damu ya Yesu inaleta huisho, utakaso, msamaha wa dhambi na kufanywa upya hata na katika maisha tuyaishio. Ndiposa twasismama na ushindi mkuu, kwani "" Ufunua wa Yohana 12:11 Nao wamemshinda kwa damu ya Mwana-Kondoo na kwa neno la ushuhuda wao, kwa kuwa wao hawakuyapenda maisha yao kiasi cha kuogopa kifo."" Damu ya Yesu yatosha!