IBADA MAALUMU YA KUMUINGIZA KAZINI MKUU WA KANISA | 21 - 01- 2024

Ibada maalumu ya kumuingiza kazini mkuu wa kanisa ASKOFU DKT. ALEX GEAHAZI MALASUSA leo tarehe 21.01.2024 . ......... ZABURI 104: 25 - 31 25. Bahari iko kule, kubwa na upana, Ndimo mlimo viendavyo visivyohesabika, Viumbe hai wakubwa kwa wadogo. 26. Ndimo zipitamo merikebu, Ndimo alimo Lewiathani uliyemwumba acheze humo. 27. Hao wote wanakungoja Wewe, Uwape chakula chao kwa wakati wake. 28. Wewe huwapa, Wao wanakiokota; Wewe waukunjua mkono wako, Wao wanashiba mema; 29 Wewe wauficha uso wako, Wao wanafadhaika; Waiondoa pumzi yao, wanakufa, Na kuyarudia mavumbi yao, 30. Waituma roho yako, wanaumbwa, Nawe waufanya upya uso wa nchi. 31. Utukufu wa BWANA na udumu milele; BWANA na ayafurahie matendo yake. UFUNUO 1: 9 - 16 9. Mimi Yohana, ndugu yenu na mwenye kushiriki pamoja nanyi katika mateso na ufalme na subira ya Yesu Kristo, nilikuwa katika kisiwa kiitwacho Patmo, kwa ajili ya neno la Mungu, na ushuhuda wa Yesu. 10. Nilikuwa katika Roho, siku ya Bwana; nikasikia sauti kuu nyuma yangu, kama sauti ya baragumu, 11. i kisema, Haya uyaonayo uyaandike katika kitabu, ukayapeleke kwa hayo makanisa saba: Efeso, na Smirna, na Pergamo, na Thiatira, na Sardi, na Filadelfia, na Laodikia. 12. Nikageuka niione ile sauti iliyosema nami. Na nilipogeuka, niliona vinara vya taa saba vya dhahabu; 13. na katikati ya vile vinara nikaona mtu mfano wa Mwanadamu, amevaa vazi lililofika miguuni, na kufungwa mshipi wa dhahabu kifuani 14. Kichwa chake na nywele zake zilikuwa nyeupe kama sufu nyeupe, kama theluji; na macho yake kama muali wa moto; 15 na miguu yake kama shaba iliyosuguliwa sana, kana kwamba imesafishwa katika tanuri; na sauti yake kama sauti ya maji mengi. 16. Naye alikuwa na nyota saba katika mkono wake wa kulia; na upanga mkali, wenye makali kuwili, ukitoka katika kinywa chake; na uso wake kama jua liking'aa kwa nguvu zake. MARKO 9: 2 - 8 2. Baada ya siku sita Yesu akawatwaa Petro, na Yakobo, na Yohana, akawaleta juu ya mlima mrefu faraghani, peke yao; akageuka sura yake mbele yao; 3. mavazi yake yakimetameta, meupe mno, jinsi asivyoweza dobi duniani kuyafanya meupe. 4. Wakatokewa na Eliya pamoja na Musa, nao walikuwa wakizungumza na Yesu. 5. Petro akajibu, akamwambia Yesu, Rabi, ni vizuri sisi kuwapo hapa; na tufanye vibanda vitatu, kimoja chako wewe, kimoja cha Musa, na kimoja cha Eliya. 6. Maana, hakujua la kunena, kwa kuwa waliingiwa na hofu nyingi. 7. Kisha likatokea wingu, likawatia uvuli; sauti ikatoka katika lile wingu, Huyu ni Mwanangu, mpendwa wangu, msikieni yeye. 8. Mara hiyo walipotazama huku na huku, hawakuona mtu pamoja nao ila Yesu peke yake. .......... 👇👇👇 // TUMIA NAMBA ZIFUATAZO KUTOA SADAKA YAKO // ▶ LIPA KWA [ M-PESA ] - 579 579 4 ▶ NAMBA YA MPESA - 0757 - 391 - 174 JINA: KKKT AZANIA FRONT CATHEDRAL MAENDELEO BANK A/C NO 0137 9274 6021 JINA: LUTHERAN CHURCH AZANIA FRONT CATHEDRAL TUFUATILIE KWENYE MITANDAO KWA TAHARIFA ZAIDI: Instagram page:   / kkkt_azaniafront_cathedral   Website: https://www.azaniafront.org/ Facebook:   / kkkt-azania-front-cathedral-101434162039079   #azaniafrontcathedral #ibada #lunchhour #morningglory #sundayservice #lutheran