TANROADS KAMILISHENI MANUNUZI BARABARA YA KISARAWE -ULEGA
Waziri wa Ujenzi, Abdallah Ulega, ameipa siku 14 Wakala wa Barabara Nchini (TANROADS) kukamilisha taratibu zote za kisheria za manunuzi, ikiwemo kumpata mkandarasi, ili kuruhusu kuanza kwa ujenzi wa barabara ya Kisarawe hadi Maneromango. Akizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika kijiji cha Masaki, Wilayani Kisarawe Mkoani Pwani, Ulega alisema Serikali imelenga kuhakikisha wananchi wanapata huduma muhimu za kijamii ikiwemo miundombinu, elimu, afya, na kilimo, hatua itakayochochea ukuaji wa uchumi. Alisisitiza kuwa Serikali inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan itaendelea kutekeleza miradi ya maendeleo, ikiwemo ujenzi wa barabara, ili wananchi wanufaike kikamilifu na fursa zilizopo. “Wana Masaki, kazi yangu leo ni moja tu—kuielekeza TANROADS kukamilisha taratibu zote za kitaalamu ili ujenzi uanze. Baada ya wiki mbili, nataka kujua ni mkandarasi gani amepatikana na yuko tayari kuanza kazi,” alisema Ulega. Aidha, Waziri huyo amewaagiza mameneja wa TANROADS na TARURA Mkoa wa Pwani kuweka utaratibu maalum wa utekelezaji wa miradi bila kukiuka sheria na taratibu, akisisitiza kuwa uwajibikaji wao utajenga imani kwa wananchi. Aliongeza kuwa kuna umuhimu wa kuweka mikakati endelevu ya miundombinu, ikiwemo uwekaji wa taa za barabarani mara baada ya ujenzi kukamilika ili kuchochea shughuli za kiuchumi hata nyakati za usiku. Katika hatua nyingine, Ulega amewaelekeza Mameneja wa TANROADS na TARURA kuandaa mpango kazi wa haraka wa ukarabati wa barabara zote zilizoharibiwa na mvua ili zirejee katika hali yake ya kawaida. Akijibu ombi la Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo, kuhusu barabara ya Dondwe–Lukwali hadi Njia Nne kurekebishwa, Waziri Ulega alielekeza wataalamu kufika eneo hilo mara moja na kuanza kazi za matengenezo bila kuchelewa.

Ulega aililia barabara ya Mkuranga, Kisarawe hadi Kibaha bungeni

RC Kunenge Awataka Wafugaji Kisarawe Kufuga Kisasa Kuinua Uchumi na Kukidhi Soko la Kimataifa

CHALAMILA ALIVYOAGIZA MWENYEKITI AKAMATWE na POLISI BAADA ya KUDAIWA KUTAPELI WATU VIWANJA....

RC HAPI AKITATUA MIGOGORO YA ARDHI MKOANI IRINGA

A Side of Jamaica The Media Won't Show You!

Nigeria: ‘Renewed Hope’ or ‘Hopelessness’? | Mehdi Hasan and Daniel Bwala | Head to Head

FULL VIDEO KILICHOMPONZA MWENYEKITI WA MTAA HADI RC CHALAMILA KUAGIZA AKAMATWE | UTAPELI WA VIWANJA.

HISTORIC COMEBACK BY THE GREATEST JAPANESE GENERATION OF ALL TIME AGAINST ANCELOTTI’S BRAZIL

Hotuba ya Mkuu wa Wilaya Mei 28, 2026

Iran war details from this week’s “CBS Evening News”

MKURUGENZI MWENDESHAJI TADB AMPA TANO WAZIRI CHONGOLO

Ego Bodybuilder HUMILIATED Beyond Belief 🤯 | Anatoly GYM PRANK

30 Reasons Why Kenya Is Not What You Expect

Great idea! A chainsaw bike that will blow your mind

Nobody Breaks Celebrities Like Rowan Atkinson

‘Extraordinary’: Judge demands Blanche put IN WRITING Trump’s “anti-weaponization” fund is dead

KATAPILA LAVAMIA NYUMBA SAA 8 USIKU LAUWA WATOTO WAWILI NA KUJERUHI BABA NA MAMA 'PEMBA'

How Traore is Magically Growing Real Apples in Desert?

Rironi–Mau Summit Highway Update 2026 | Massive Progress on Kenya's Biggest Road Project

