Maalim Seif atangaza kuhamia ACT Wazalendo

Nchini Tanzania mwelekeo mpya wa kisiasa umejitokeza baada ya aliyekuwa katibu mkuu wa chama cha wananchi Cuf, Maalim Seif Shariff kutangaza kujiunga na chama kingine cha upinzani, ACT Wazalendo. Ni baada ya Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Dar es Salaam kukubaliana na uamuzi wa Msajili wa Vyama vya Siasa kumtambua Profesa Ibrahim Lipumba kuwa Mwenyekiti halali wa Chama cha Wananchi (CUF).Ahmad Juma ametuandalia vidio hii. Kurunzi 18.03.2019