SERIKALI YAHIMIZA USIMAMIZI BORA WA GHALA KUINUA BIASHARA YA MAZAO
Watumishi na wasimamizi wa shughuli za ghala nchini wametakiwa kutekeleza majukumu yao kwa uadilifu, weledi na uwajibikaji ili kuimarisha Mfumo wa Stakabadhi za Ghala na kuongeza ufanisi katika biashara ya mazao ya kilimo. Wito huo umetolewa na Afisa Tawala wa Wilaya ya Morogoro, Bi. Janeth Chatta, kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, alipokuwa akifunga mafunzo ya wasimamizi wa shughuli za ghala kwa msimu wa biashara wa mbaazi na dengu 2026/2027 yaliyofanyika wilayani humo. Bi. Chatta amesema uadilifu wa watendaji wa mfumo ni msingi wa kujenga imani kwa wakulima, wanunuzi na taasisi za fedha, huku akisisitiza kuwa Mfumo huo umeendelea kuwa nyenzo muhimu ya kuhakikisha biashara ya mazao inafanyika kwa uwazi, ubora na ushindani. Amesema Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan inaendelea kuhimiza matumizi ya Mfumo huo pamoja na Soko la Bidhaa Tanzania (TMX) ili kuongeza thamani ya mazao, masoko yenye ushindani na manufaa kwa wakulima. Amewataka washiriki kutumia maarifa waliyopata kutekeleza majukumu yao kwa weledi, kuendana na mabadiliko ya teknolojia na kuhakikisha taarifa za mazao zinakuwa sahihi na kwa wakati. Pia ameipongeza Bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala (WRRB) kwa kuendelea kuimarisha uwezo wa watendaji kupitia mafunzo yanayochangia kuongeza ufanisi wa mfumo na kukuza biashara ya mazao nchini. Mafunzo hayo yamefanyika kwa siku tano kuanzia na yamehudhuriwa na washiriki 103 kutoka kampuni za uendeshaji ghala na wadau mbalimbali wa mfumo.

MWITA:ZINGATIENI KANUNI NA SHERIA PAMOJA NA UADILIFU

NGEC Yataka Ulinzi Imara Zaidi kwa Watetezi wa Mazingira Wanawake Kufuatia Kuongezeka kwa Vitisho

This Man Failed At The Life He Had Planned, Then Built A Better One In His Village | Nasto | LNN

She Built a Million Dollar Farm Empire in 12 Months

WRRB YAWAJENGEA UWEZO WATENDAJI WA GHALA, MSIMU WA MBAAZI NA DENGU

BANGU: TUNAUNGANISHA BIASHARA YA MIFUGO KIDIGITALI KUPITIA MFUMO WA STAKABADHI ZA GHALA

DW Kiswahili Habari za Ulimwengu | Podcast | Dunia Yetu | Leo Asubuhi | 15.07.2026 | Swahili News

HIVI NDIVYO WATAALAM KUTOKA WRRB WALIVYOTATUA CHANGAMOTO YA UFUTA ULANGA MOROGORO

She Left IT to Run a 20-Acre Mango Farm | How Hendy Farms Makes Money Through Value Addition

WATAALAM WA AFYA WILAYA YA KILINDI WAPATIWA MAFUNZO YA AFYA MAONI

Madiwani Chamwino Wapatiwa Elimu Kukabiliana na Kujikinga na Ugonjwa wa Ebola

WRRB YAANZA KUTEKELEZA MAAGIZO YA WAZIRI MKUU

🟠Ol Kalou Chaos: A Dark Dress Rehearsal for 2027? With Analyst Gatonye Wa Mbugua Magathiti

WHAT A MAN! Listen to President Ruto's Great speech as he hosts AFC Leopards Team at State House

CAMFED YAUNGA MKONO JUHUDI ZA SERIKALI KATIKA SEKTA YA ELIMU

EABC–TCCIA AGRA Project Beneficiary Testimonial I Esther Wausi

KILIMO AJIRA YANGU:TARI ILONGA WATAFITI MBEGU BORA KUKABILIANA NA MABADILIKO YA TABIANCHI 19.04.2025

| SUNDAY LIVE | BACK TO THE FRONTLINES | TONY GACHOKA

I left a life of luxury in America, only to come and live in isolation in Kenya | Tuko TV

