RAIS SAMIA ATOA KIBALI WATUMISHI WA UMMA 219,042 KUPANDISHWA VYEO 2025/26

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na utawala bora Mhe. Ridhiwan Jakaya Kikwete amemshukuru Rais wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuendelea kupandisha vyeo watumishi wa umma, akisema kwa mwaka 2025/26, Rais Samia ametoa kibali cha kupandisha vyeo watumishi 219,042. Waziri Ridhiwan Kikwete amebainisha hayo leo Jumatano Mei 06, 2026 Jijini Arusha kwenye Kitui cha Mikutano cha AICC, wakati wa ufunguzi wa mkutano wa pili wa Jumuiya za Wataalamu wa utawala na rasilimaliwatu, Tawi la Tanzania, akisema hatua ya upandishaji vyeo ni utekelezaji wa nia ya Rais Samia ya kuboresha maslahi ya Watumishi na kuacha tabasamu kwa Watanzania. "Matarajio yangu kwa idadi hii tuliyopewa, kama waziri nataka kuiona furaha hiyo, kila sehemu nitakapokwenda na ukisikia ninakuja Mkoani kwako ile taarifa nitakayopewa ya utendaji kazi katika eneo la rasilimali watu ndani yake utoe taarifa ni wangapi umewapandisha vyeo. Taarifa yako ikiwa haina jambo hilo nikuhakikishie tukimaliza nitaondoka na wewe." Amesisitiza Waziri Ridhiwani. Waziri Ridhiwani kadhalika amesisitiza Maafisa hao kuendelea kuzingatia muongozo wa kujitolea katika utumishi wa umma wa mwaka 2025 ili kuendelea kutoa nafasi kwa vijana wenye sifa kwa njia ya uwazi na haki kutegemeana na nafasi katika maeneo yao ya kazi, akisisitiza pia umuhimu wa Maafisa hao kujitathimini namna ambavyo wanaweza kuwa sehemu ya mageuzi kiutendaji kwa lengo la kuboresha huduma na kupunguza malalamiko yasiyokuwa ya lazima kutoka kwa wananchi. Waziri Ridhiwani pia amewataka Maafisa rasilimali watu kutekeleza wajibu wao kama wasimamizi wa utawala na rasilimaliwatu katika utumishi wa umma kwa kukamilisha yale yanayopaswa kutekelezwa katika ngazi ya Taasisi zao, badala ya kuongeza mzigo kwa Mamlaka kwa kushughulikiwa kwa wakati katika ngazi ya Taasisi, akisema ni matarajio yake kuwa mwezi Mei 2026 wakati wa zoezi la upandishaji vyeo wale wote ambao wamekidhi vigezo na kutengewa bajeti watapandishwa kwa wakati. Awali katika maelezo yake Rais wa Jumuiya za wataalamu wa utawala na rasilimaliwatu (AAPAM Afrika) Dkt. John Nakabago amesema katika mkutano huo wa siku mbili utajadili masuala mbalimbali ikiwemo mageuzi ya utumishi wa umma katika zama za kidijitali na namna bora ya kusimamia rasilimali watu katika namna bora. Kwa upande wake Katibu tawala wa Mkoa wa Arusha Dkt. Toba Alnason Nguvila, akimuwakilisha Mkuu wa Mkoa katika Mkutano huo ameeleza kutambua mchango wa Maafisa rasilimaliwatu, akisisitiza kutekeleza maagizo yote yaliyotolewa na Waziri Kikwete.

🇪🇹 Once Neglected, Ethiopia's Mining Sector Is Now a Growth Engine | Eng. Hanna Berhanu
▶︎

🇪🇹 Once Neglected, Ethiopia's Mining Sector Is Now a Growth Engine | Eng. Hanna Berhanu

WATUMISHI WAPYA SEKRETARIETI YA AJIRA WATAKIWA KUZINGATIA SHERIA NA KANUNI
▶︎

WATUMISHI WAPYA SEKRETARIETI YA AJIRA WATAKIWA KUZINGATIA SHERIA NA KANUNI

"Hizi ndio sababu za kupata promosheni/vyeo/ recategorization kwa watumishi wa Umma" Dr Francis
▶︎

"Hizi ndio sababu za kupata promosheni/vyeo/ recategorization kwa watumishi wa Umma" Dr Francis

Ecuador vs. Germany Highlights FIFA World Cup 2026 | Sportschau
▶︎

Ecuador vs. Germany Highlights FIFA World Cup 2026 | Sportschau

የሀገር በቀል ማክሮ-ኢኮኖሚ ማሻሻያው ስኬት እና የብሔራዊ ባንክ ገዥ ማብራሪያ | Macro-Economic Reform Ethiopia | NBE Governor
▶︎

የሀገር በቀል ማክሮ-ኢኮኖሚ ማሻሻያው ስኬት እና የብሔራዊ ባንክ ገዥ ማብራሪያ | Macro-Economic Reform Ethiopia | NBE Governor

MWALIMU ASIMULIA ALIVYOKATWA MKONO NA MUMEWE, WATOTO WAKE WAONE VIDOGOLE VILIVYOKATWA, WANAFUNZI
▶︎

MWALIMU ASIMULIA ALIVYOKATWA MKONO NA MUMEWE, WATOTO WAKE WAONE VIDOGOLE VILIVYOKATWA, WANAFUNZI

OUTSIDER POLITIC #3. Constantin Toma: „Nu Grindeanu conduce PSD, ci familia Olguța - Claudiu”
▶︎

OUTSIDER POLITIC #3. Constantin Toma: „Nu Grindeanu conduce PSD, ci familia Olguța - Claudiu”

Watumishi wa Umma 193,166 Kupandishwa Madaraja Mei Mosi
▶︎

Watumishi wa Umma 193,166 Kupandishwa Madaraja Mei Mosi

11th Our Ocean Conference Closing Ceremony
▶︎

11th Our Ocean Conference Closing Ceremony

CAG MSTAAFU PROFESA ASSAD AFUNGUKA SABABU ZILIZOPELEKEA KUONDOLEWA KATIKA NAFASI YA CAG
▶︎

CAG MSTAAFU PROFESA ASSAD AFUNGUKA SABABU ZILIZOPELEKEA KUONDOLEWA KATIKA NAFASI YA CAG

BAADA YA MAAMUZI YA RAIS SAMIA KWA WATUMISHI WALIOFUKUZWA KWA VYETI FEKI.
▶︎

BAADA YA MAAMUZI YA RAIS SAMIA KWA WATUMISHI WALIOFUKUZWA KWA VYETI FEKI.

DC KALLI AINGILIA KATI KERO ZA MADEREVA WA MALORI LONGIDO
▶︎

DC KALLI AINGILIA KATI KERO ZA MADEREVA WA MALORI LONGIDO

HAFLA YA KUFUNGA MAFUNZO YA AWALI YA ASKARI WA ZIMAMOTO KOZI NAMBA 6/2026
▶︎

HAFLA YA KUFUNGA MAFUNZO YA AWALI YA ASKARI WA ZIMAMOTO KOZI NAMBA 6/2026

What UN Officials Keep Asking About Ethiopia’s Growth – Claver Gatete Speaks
▶︎

What UN Officials Keep Asking About Ethiopia’s Growth – Claver Gatete Speaks

Ethiopia is About to Explode.
▶︎

Ethiopia is About to Explode.

WAZIRI RIDHIWANI KIKWETE ATOA MAAGIZO KWA WATUMISHI WA UMMA NCHINI,AWATAKA KUTOJIKWEZA WATENDE HAKI
▶︎

WAZIRI RIDHIWANI KIKWETE ATOA MAAGIZO KWA WATUMISHI WA UMMA NCHINI,AWATAKA KUTOJIKWEZA WATENDE HAKI

NAIBU KATIBU MKUU UTUMISHI AKEMEA MIUNGUWATU KWA MAAFISA RASILIMALIWATU NA UTUMISHI
▶︎

NAIBU KATIBU MKUU UTUMISHI AKEMEA MIUNGUWATU KWA MAAFISA RASILIMALIWATU NA UTUMISHI

PRESIDENT SAMIA APPROVES PROMOTIONS FOR 219,042 EMPLOYEES FOR THE 2025/2026 FINANCIAL YEAR
▶︎

PRESIDENT SAMIA APPROVES PROMOTIONS FOR 219,042 EMPLOYEES FOR THE 2025/2026 FINANCIAL YEAR