WATUMISHI WAPYA SEKRETARIETI YA AJIRA WATAKIWA KUZINGATIA SHERIA NA KANUNI
Watumishi wapya wa Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma wametakiwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu za utumishi wa umma katika utendaji wao. Wito huo umetolewa na Mhasibu Mkuu wa Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma Christopher Nkupama (CPA) wakati akifungua mafunzo ya awali Kwa watumishi wapya kwa niaba ya Kaimu Katibu wa Ofisi hiyo. "Ndugu washiriki, mkiwa watumishi wa umma mara zote mnapaswa kujua na kuzingatia sheria na kanuni mbalimbali za utumishi wa umma" alisema Nkupama. Aidha, katika ufunguzi huo, Mhasibu Nkupama ameeleza kuwa Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma ina matarajio makubwa kwa watumishi hao katika kuhakikisha wanaongeza ufanisi wa kiutendaji. "Tuna matarajio kuwa mtakapofahamu sheria na taratibu mtaongeza ufanisi katika utendaji na uwajibikaji utakuwa mkubwa, kwa kuwa sisi tunawajibika Kwa wananchi na wadau wetu wengine basi mafunzo haya yakatuongezee kitu katika kuwasaidia wananchi" aliongeza. Katika hatua nyingine Mhasibu Mkuu huyo wa Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Ajira amewapongeza watumishi wapya wa Ofisi hiyo na kuwasisitiza kutekeleza wajibu wao ipasavyo ili kumsaidia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan kutimiza malengo ya serikali kwa kutoa huduma bora kwa wananchi. Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Chuo Cha Utumishi wa Umma, Mkurugenzi wa Chuo hicho kutoka ndaki ya Singida Dkt.Hamis Amani ameupongeza uongozi wa Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma kwa kuandaa mafunzo hayo kwa watumishi wapya wa ofisi hiyo. "Nawapongeza kwa kuandaa mafunzo haya ambayo yatawafanya washiriki wawe na uelewa wa kina kuhusu utumishi wa umma na kutambua sheria na miongozo ya Utumishi wa umma" alifafanua Dkt.Amani. Vilevile Dkt.Amani amewataka watumishi hao kuzingatia mafunzo hayo ili kutokwamisha utendaji wa serikali na kuchelewesha huduma kwa wananchi. Mafunzo elekezi ya awali kwa watumishi wapya wa Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma yanafanyika Kwa siku tatu kuanzia Agosti 28 hadi Agosti 30, 2023 jijini Dodoma.

MAMBO MATANO YA KUZINGATIA KABLA YA KUOMBA KAZI KWENYE AJIRA PORTAL

OUTSIDER POLITIC #3. Constantin Toma: „Nu Grindeanu conduce PSD, ci familia Olguța - Claudiu”

KATIBU MKUU UTUMISHI, AWAONYA MAMENEJA RASILIMALI WATU

MATOKEO YA USAILI WA MAHOJIANO (ORAL) NA WALIOPO KWENYE KANZIDATA KUANZA KUWEKWA WAZI HIVI KARIBUNI

MUOMBAJI AJIRA AEPUKE MAMBO HAYA ILI AFANIKIWE

SEKRETARIETI YA AJIRA KUZINDUA MFUMO MPYA WA USAILI

Serikali yasema mgawanyo wa ajira za walimu unazingatia utaifa

MAMBO MUHIMU YA YANAYOZINGATIWA KATIKA MCHAKATO WA AJIRA

FAHAMU KUHUSU KANZIDATA (DATABASE) YA SEKRETARIETI YA AJIRA

Afisa Utumishi Mkuranga atuhumiwa kuomba rushwa ya ngono kwa Watendaji wa Vijiji

MAELEKEZO YA NAMNA YA KUTUMIA HUDUMA YA UHAMISHO KWENYE DIRISHA LA WATUMISHI PORTAL

MBUNGE SHABIBY AFUNGUKA "NILINUNUA BASI LA KWANZA NIKIWA NA MIAKA 19"

Ecuador – Deutschland Highlights | Gruppe E, FIFA WM 2026 | sportstudio

SEKRETARIETI YA AJIRA NI LANGO LA KUINGILIA UTUMISHI WA UMMA MHE DEUS SANGU

SIFA ZA MSAILIWA KUWEKWA KWENYE KANZIDATA/ DATABASE

BIBI wa SUMBAWANGA amvaa WAZIRI MKUU MWIGULU kwa madai haya MAZITO "sitaki kiwanja nataka hela"

UFAHAMU MCHAKATO WA AJIRA

MAKALA : SIKU 100 ZA MHE. RAIS DKT SAMIA SULUHU HASSAN SEKTA YA AJIRA (AJIRA 12,000)

Ethiopia is About to Explode.

