MBOLEA ZA ORGANIC ZAPIGIWA CHAPUO
Kupitia maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Kibiashara sabasaba, Wadau wa kilimo wameelezea namna wameendelea kuimarisha juhudi za kuongeza tija katika sekta ya kilimo kupitia kuendeleza kilimo ikolojia hai, kuhamasisha matumizi ya mbolea za organic na bidhaa za kibailojia, pamoja na kuwawezesha vijana kushiriki katika kilimo biashara. Mratibu wa Tanzania Organic Agriculture Movement (TOAM), Ernest Jerome, alisema Tanzania tayari ina Mkakati wa Taifa wa Kilimo Ikolojia Hai unaolenga kuboresha upatikanaji wa pembejeo, kuongeza ushirikiano wa wadau na kuwainua wakulima kupitia kilimo endelevu. Wakati huo huo, Serikali kupitia Wizara ya Kilimo, TFRA na Tanzania Fertilizer Company (TFC) inaendelea kushirikiana na wazalishaji wa mbolea za organic na bidhaa za kibailojia ili kuongeza uzalishaji wa pembejeo zinazotengenezwa nchini na kupunguza utegemezi wa bidhaa kutoka nje. Kwa upande wake, Meneja Masoko wa Tanzania Biotech Product Limited (TBPL), Samuel Ponziray, alisema bidhaa za kibailojia zinazozalishwa na kiwanda hicho zimeendelea kusaidia kudhibiti mazalia ya mbu na kuchangia kupungua kwa kiwango cha maambukizi ya malaria nchini kutoka asilimia 14.3 hadi asilimia 5.5, huku Serikali ikilenga kutokomeza malaria ifikapo mwaka 2030. Aidha, Wizara ya Kilimo imewahimiza vijana kutumia fursa za BBT Project One, programu inayotoa mafunzo ya kilimo biashara, mashamba ya pamoja, ufugaji na uwezeshaji wa kifedha ili kuongeza ushiriki wa vijana katika sekta ya kilimo na kuifanya kuwa chanzo cha ajira na ukuaji wa uchumi.

From the Streets to Building a Successful Life in the Village| Mayuguno’s Story of Survival &Success

RESTORING THE ORDER JULY 2026 - DAY 6 #dunsinoyekan #worship #intimacy

I started with one cow now I have 150 High Grade cows producing 1000L of milk daily& I rear chicken

MAKONGORO NYERERE

WIKI YA FEDHA JIJINI TANGA

Growing Avocados In Containers and Getting Fruit

NFRA: CHAKULA KIPO CHA KUTOSHA MARA NNE YA IDADI INAYO TAKIWA

Why We're Digging Trenches To Plant Mangroves

LIVE : RIPOTI NZITO YA LHRC YAFICHUA UKWELI WA OKTOBA 29 – na yote ya 2025

🔴#LIVE: TEC WANATOA TAMKO YALIYOTOKEA OKTOBA 29 ,NA MSIMAMO MKALI...

LES DEFIS DE LA SECURITE ALIMENTAIRE -Thione NIANG #JEUFZONE Farm

UWEKEZAJI BANDARI YA DAR ES SALAAM

He Left the Food System to Build This!

Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi Tanzania (TAFIRI),Dkt. Ismael Kimirei akizungumza TBC

How She Started A Profitable Poultry Farm with 300 Chicks!

JE UNAFAHAMU WATU WOTE DUNIANI WALITOKEA NGOROGORO?

SABASABA 2026 DIB NA AFI GREEN: WADAU NJOONI TUYAJENGE

UBUNIFU WA TEKNOLOJIA ZA VETA WAVUTA HISIA ZA WENGI SABASABA 2026

I Went to China to Buy a $5,000 Modular Home — What's the Real Cost?

