TAZAMA: MWENGE WA UHURU WILAYANI MUHEZA

Mwenge wa uhuru wilayani Muheza mkoani Tanga umekagua, umezindua , kutembelea na kuweka jiwe la msingi miradi nane yenye thamani ya shilingi bilioni 5. 6 Miradi hiyo ya maendeleo ni pamaja na afya , maendeleo ya jamii, utunzaji wa Mazingira, barabara,uchumi pamoja na sekta binafsi. Akizungumza katika mradi wa ujenzi wa daraja ( Box Culvert) mkimbiza mwenge kitaifa Abdallah Shaibu Kaimu ameipongeza Serikali ya awamu wa sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kazi kubwa na nzuri anayoifanga kwa wananchi wake kuwaletea miradi mikubwa ya maendeleo ambayo inaondao changamoto katika maeneo yao. Kwa upande mbunge wa Muheza Mhe. Hamis Mwinjuma amesema ujenzi wa daraja hilo ni mkombozi mkubwa kwa wakazi wa vijiji vya Zeneti, Bwiti na Kimbo kuwaunganisha katika shughuli za kiuchumi hasa katika nyakati za mvua. Nao baadhi ya wananchi wa vijiji hivyo wamemshukuru Rais Dkt. Samia Samia kwa kuwapa fedha na kuhakikisha daraja hili linakamilika kwa wakati ili kuondoa adha kubwa waliyokuwa wanaipata hasa katika kipindi cha mvua.