RC TANGA APONGEZA MRADI WA MIFUGO MRUAZI KUINUA VIJANA

Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe. Balozi Dkt. Batilda Burian, amewapongeza waendeshaji wa shamba la mifugo la Mruazi kwa juhudi zao za kuzalisha mitamba bora ya maziwa inayosaidia kuwainua wafugaji wadogo na vijana kiuchumi. Akizungumza wakati wa ziara yake katika shamba hilo lililopo wilayani Korogwe, Balozi Batilda amesema mradi huo unachangia kwa kiasi kikubwa kuongeza uzalishaji wa maziwa, ajira kwa vijana, na kukuza uchumi wa mkoa. Amesisitiza kuwa juhudi hizo zinaunga mkono maono ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuwajengea vijana kesho iliyo bora kupitia sekta za uzalishaji. Ameeleza kuwa kupitia mradi huo, vijana wanapatiwa ardhi, nyumba na mifugo, hali inayowawezesha kuanza ufugaji wa kisasa na kurejesha mikopo kwa urahisi huku wakiongeza kipato chao. Balozi batilda amesisitiza kuwa Serikali ya Mkoa wa tanga itaendelea kushirikiana na taasisi mbalimbali zinazohusika na mradi huo kuhakikisha mafanikio ya mradi huo yanaongezeka na kuwanufaisha wananchi wengi zaidi. Kwa upande wake, msimamizi wa kitalu cha mfano katika shamba hilo, Selemani Mwedi, amesema walianza uzalishaji mwaka 2024 wakiwa na mitamba mitano pekee, lakini hadi sasa wamefanikiwa kuongeza idadi ya ng’ombe hadi kufikia nane pamoja na kuanza uzalishaji wa maziwa unaofikia lita 60 kwa siku. Ameongeza kuwa maendeleo hayo yamewasaidia kuanza kurejesha walioupata kwa ajili ya kuendesha shughuli hizo. Naye mhasibu wa shamba hilo, Rehema Shekimweli, amesema kampuni hiyo ilianza uwekezaji rasmi mwaka 2009 ikiwa na lengo la kuzalisha mitamba bora ya kisasa kwa ajili ya wafugaji wadogo. Ameeleza kuwa hadi sasa shamba lina uwezo wa kuzalisha mitamba 150 kwa mwaka, lita 900,000 za maziwa, pamoja na madume bora ya mbegu na nyama kwa ajili ya soko la ndani. Mradi huo unatarajiwa kupanuliwa zaidi ili kuwafikia vijana wengi zaidi, huku lengo likiwa ni kufikia vijana 100 watakaonufaika moja kwa moja na kuwa mfano wa wafugaji wa kisasa nchini.

KILA KIPANDE CHA ARDHI JIJI LA TANGA KITAPATIWA  HATI.
▶︎

KILA KIPANDE CHA ARDHI JIJI LA TANGA KITAPATIWA HATI.

JIJI LA TANGA NA KILIMO CHA MWANI.
▶︎

JIJI LA TANGA NA KILIMO CHA MWANI.

She Was Trying to Cut It With Scissors and The Grass Was Taller Than My Mowers
▶︎

She Was Trying to Cut It With Scissors and The Grass Was Taller Than My Mowers

RC BATILDA AKAGUA UJENZI WA MKWAKWANI PLAZA, AHIMIZA WANATANGA KUCHANGAMKIA FURSA
▶︎

RC BATILDA AKAGUA UJENZI WA MKWAKWANI PLAZA, AHIMIZA WANATANGA KUCHANGAMKIA FURSA

Mahubiri ya Askofu Jackson Sosthenes Jackson wa Kanisa Anglikana Tanzania Dayosisi ya Dar es Salaam
▶︎

Mahubiri ya Askofu Jackson Sosthenes Jackson wa Kanisa Anglikana Tanzania Dayosisi ya Dar es Salaam

DHAMIRA YA DK.MWINYI KUIFUNGUA PEMBA KIUCHUMI INAONEKANA KIVITENDO
▶︎

DHAMIRA YA DK.MWINYI KUIFUNGUA PEMBA KIUCHUMI INAONEKANA KIVITENDO

RC TANGA AUNDA KAMATI KUCHUNGUZA UVUNJWAJI WA NYUMBA KIJIJI CHA MSAKANGOTO, MUHEZA
▶︎

RC TANGA AUNDA KAMATI KUCHUNGUZA UVUNJWAJI WA NYUMBA KIJIJI CHA MSAKANGOTO, MUHEZA

Earn Ksh 2 Million Per Acre with Hybrid Sukuma Wiki: A Farmer's Success Story
▶︎

Earn Ksh 2 Million Per Acre with Hybrid Sukuma Wiki: A Farmer's Success Story

ASMR Addictive Fast Tapping Collection For Deep Sleep & Anxiety Relief (No Talking) — 2.5 Hours
▶︎

ASMR Addictive Fast Tapping Collection For Deep Sleep & Anxiety Relief (No Talking) — 2.5 Hours

''ZANZIBAR IPEWE NAFASI'' MBUNGE KING ashusha PONTI kuhusu MUUNGANO
▶︎

''ZANZIBAR IPEWE NAFASI'' MBUNGE KING ashusha PONTI kuhusu MUUNGANO

WADAIWA WA KODI YA PANGO LA ARDHI TANGA WAANZA  KUPELEKWA MAHAKAMANI
▶︎

WADAIWA WA KODI YA PANGO LA ARDHI TANGA WAANZA KUPELEKWA MAHAKAMANI

TAHARUKI: WANANCHI WA MICHENZANI BLOCK NO (2) WALIA NA KERO YA MAJI MACHAFU.
▶︎

TAHARUKI: WANANCHI WA MICHENZANI BLOCK NO (2) WALIA NA KERO YA MAJI MACHAFU.

RC TANGA AKAGUA MADHARA YA MVUA NA UPEPO MSOMERA, ATOA MAAGIZO KUREJESHA HUDUMA MUHIMU
▶︎

RC TANGA AKAGUA MADHARA YA MVUA NA UPEPO MSOMERA, ATOA MAAGIZO KUREJESHA HUDUMA MUHIMU

WAKULIMA MINJINGU WAPEWA ELIMU  KUHUSU NJIA RAHISI ZA KUDHIBITI NDEGE NA WANYAMA WAHARIBIFU
▶︎

WAKULIMA MINJINGU WAPEWA ELIMU KUHUSU NJIA RAHISI ZA KUDHIBITI NDEGE NA WANYAMA WAHARIBIFU

TAMASHA LA ASKOFU NA VIJANA 2025 KKKT-DKMs
▶︎

TAMASHA LA ASKOFU NA VIJANA 2025 KKKT-DKMs

How To Turn a Small Land Into Millions( Even If you are Lazy): 6 Secrets Revealed!
▶︎

How To Turn a Small Land Into Millions( Even If you are Lazy): 6 Secrets Revealed!

TANGA YAJIPANGA KUWA KITOVU CHA UTALII MIKOA YA   KASKAZINI  NA ZANZIBAR
▶︎

TANGA YAJIPANGA KUWA KITOVU CHA UTALII MIKOA YA KASKAZINI NA ZANZIBAR

Inside a 150-Cow Dairy Farm Producing 1,000 Litres of Milk Daily 🐄🥛🔥| Njenga Mabati DY Farm Kenya
▶︎

Inside a 150-Cow Dairy Farm Producing 1,000 Litres of Milk Daily 🐄🥛🔥| Njenga Mabati DY Farm Kenya

Makampuni 408 Yaruhusiwa Rasmi Kusafirisha Mazao na Bidhaa za Kilimo Kwenda Nchini China
▶︎

Makampuni 408 Yaruhusiwa Rasmi Kusafirisha Mazao na Bidhaa za Kilimo Kwenda Nchini China

MWAFAKA WAIVA ZANZIBAR,SERIKALI YA UMOJA WA KITAIFA (SUKI) MBIONI KUREJEA
▶︎

MWAFAKA WAIVA ZANZIBAR,SERIKALI YA UMOJA WA KITAIFA (SUKI) MBIONI KUREJEA