RC MTWARA ASHANGAZWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MASASI MJI "HALMASHAURI NYINGINE WAJE KUJIFUNMASADI"
RC MTWARA ASHANGAZWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI MASASI MJI, AZITAKA HALMASHAURI NYINGINE KUJA KUJIFUNZA MASASI Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe. Kanali Patrick Sawala ameshangazwa na utendaji kazi wa kasi ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo unaofanywa na Mkurugenzi wa Mji Masasi Ndg. Reuben Sixbert Jichabu na watalaamu wake kwa kukamilisha miradi kwa wakati na ubora unaostahili huku akimuagiza Katibu Tawala Mkoa kuzileta Halmashauri zinazosuasua katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo kuja kujifunza Halmashauri ya Mji Masasi. Mhe. Mkuu wa Mkoa amesema hayo leo 21 Juni, 2024 wakati wa ziara yake ya kuzungumza na watumishi sambamba na kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo wilayani Masasi hususani ujenzi wa vyumba vinne vya madarasa na matundu nane ya vyoo katika shule ya sekondari Anna Abdallah. “ Natambua uwepo wa Mwenyekiti wetu wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Masasi, viongozi na watu wote, nashindwa niseme nini lakini jamani kuna watu wanatenda kazi, fedha imepokelewa tarehe 3/4/2024 leo jengo lipo hivi, nitoe shukurani na pongezi za dhati kwako Mhe,Mkuu wa Wilaya lakini Mkurugenzi na Timu yako yote ambayo inakusaidia katika uratibu, lakini wasimamizi kuanzia ngazi ya walimu, viongozi wa kata na wananchi wote kwa ujumla wake kwa kazi nzuri kama hii, RAS nikuombe katika wale ambao wanaosuasua katika miradi walete waje wajifunze Masasi, kazi ni nzuri”, Mhe Mkuu wa Mkoa. Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Masasi, Ndg. Reuben Sixbert Jichabu amesema mbali na Ujenzi wa vyumba vinne vya madarasa na matundu nane ya vyoo katika Shule ya Sekondari Anna Abdallah, siku hiyohiyo tarehe 3/4/2024 fedha ilipokelewa Masasi Day kwaajili ya Ujenzi wa madarasa matatu na matundu nane ya vyoo sambamba na Nangose, darasa moja na matundu nane ya vyoo ambapo shule hizo mbili ujenzi wake umekamilika kwa kila kitu kinachosubiriwa ni wanafunzi kuingia darasani kusoma. Awali akisoma taarifa ya ujenzi wa mradi huo, Makamu Mkuu wa Shule ya Sekondari Anna Abdallah, Mwl, Zamoyoni Adam amesema shule hiyo ilipokea fedha kutoka Serikali kuu tarehe 3/4/2024 zaidi ya shilingi milioni 110 kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vinne vya madarasa na matundu nane ya vyoo. Amesema utekelezaji wa mradi huo ulianza tarehe 20/4/2024 na kwa mujibu wa mkataba unatakiwa kukamilika 20/7/2024 lakini kutokana na kasi ya utekelezaji wa mradi mradi huo unatarajiwa kukamilika kabla au ifikapo 28/6/2024. Aidha ametoa shukurani zake kwa Serikali katika kuhakikisha Mazingira ya ujifunzaji na ufundishaji shuleni yanaboreshwa. “Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa Jumuiya ya Shule ya Secondari Anna Abdallah inatoa shukurani zake za dhati kwa Mhe. Dkt, Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuboresha miundombinu ya Shule ya Sekondari ili kutengeneza Mazingira mazuri ya ujifunzaji na ufundishaji mashuleni , Aidha jumuiya ya Shule ya sekondari inaendelea kutoa shukurani zake kwa Mhe. Geoffrey Mwambe, Mbunge wa Jimbo la Masasi Mjini na Mhe. Sospeter Nachunga, Diwani kata ya Napupa kwa ushirikiano wao mkubwa wanaoutoa katika utekelezaji wa mradi”.

WANANCHI WAIBUA MADUDU HOSPITALI YA LIGULA MTWARA RC SAWALA AAHIDI KUCHUKULIWA HATUA KWA WAHUSIKA

Halmashauri ya Mji wa Masasi kujenga stendi kuu eneo la TUKULA

18 June 2026

RC MTWARA AKEMEA UZEMBE (CAG)

RC MTWARA AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO NANYAMBA TC

MSTAAFU ALIYEAMUA KUHAMIA KWENYE UFUGAJI WA SAMAKI

BODABODA MASASI WALALAMIKA KUHUSU WIZI/TUNAFANYA KAZI MWISHO SAA KUMI NA MBILI

MKUTANO WA HADHARA UWANJA WA BOMANI - MASASI MJI

MALIPO YA WAKULIMA CHAMA KIKUU MAMCU MTWARA

HALMASHAURI YA MJI MASASI YAPEWA SIFA KWA UFUNGAJI BORA WA HESABU 2024/2025.

WAHASIBU WATATU H/ MJI MASASI WASIMAMISHWA KAZI KWA KUGHUSHI VIBALI, RISITI

UKARABATI WA UWANJA WA BOMANI MASASI WAANZA RASMI

JANITOR vs THE BIGGEST GUYS IN THE GYM. They Didn’t Expect THAT

MBUNGE WA MASASI MJINI GEOFFREY MWAMBE AELEZA MIPANGO YA KUMALIZA TATIZO LA UMEME MASASI

JUMUIYA YA WAZAZI CCM MKOA WA MTWARA WAJITOKEZA KUPANDA MITI NA USAFI KITUO CHA AFYA MIKANGAULA

Samaki wa uzito wa Kg 2154.9 wamevuliwa na walengwa wa mpango wa kunusuru kaya maskini Ilemela

Waziri Mkuu awasimamisha kazi maafisa wa Halmashauri ya Mji Masasi

Masasi Town Councilors enjoy learning visit to Kibaha Municipal Council

Mlima Mkomaindo Fursa ya Utalii Masasi

