MHE AYOUB: KILIMO CHA MPUNGA KISIMAMIWE KITAALAMU, SI KISIASA
Viongozi wa Jimbo la Chaani wameanza hatua za kuweka mfumo mpya wa kuimarisha kilimo cha mpunga kwa kuvisimamia vikundi vya wakulima kitaalamu, hatua inayolenga kukifanya kilimo hicho kuwa endelevu na kuwa chanzo cha ajira kwa vijana. Akizungumza katika kikao na wakulima wa mpunga wa Jimbo hilo, Mbunge wa Chaani ambaye pia ni Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Ayoub Mohamed Mahmoud, alisema hatua iliyopo sasa ni kuhakikisha vikundi vya wakulima vilivyoundwa vinasajiliwa na kupewa usimamizi wa kitaalamu ili kuweka msingi imara wa maendeleo ya sekta hiyo. Alisema ili kusaidia sekta ya kilimo kwa ufanisi, ni lazima isimamiwe kwa mtazamo wa kitaalamu zaidi na kuwekwa mikakati thabiti itakayohakikisha inaendelea kuwa na tija kwa muda mrefu. "Tupo kwenye hatua ya utekelezaji, tumeshaunda vikundi na sasa tupo kwenye hatua ya kuvisajili. Kama tunataka kuwasaidia wakulima kiukweli lazima tusimamie jambo hili kitaalamu na si kufanya siasa. Tunataka sekta hii ya kilimo iwe endelevu," alisema Mhe. Ayoub. Alisema uendelevu wa kilimo unamaanisha kujenga mazingira yatakayowezesha sekta hiyo kuzalisha ajira ndani yake, ambapo vijana wataweza kuona kilimo kama fursa ya ajira na kipato badala ya shughuli inayofanywa na wazee pekee. "Tutengeneze ajira ndani ya hiki hiki kilimo mnacholima, watoto wetu watengenezewe ajira humu humu. Ajira hizo zitatengenezwa vipi? Ndiyo maana tumewaletea wataalamu," aliongeza.

'Unataka Tufunguliwe Kesi za Uhaini na Ugaidi?': CHADEMA Wamjibu Nchimbi Kuhusu Kudai Katiba Mpya

'Pambaneni Mpate Katiba Mpya! Tukomae Hapo Hapo': Kauli ya Makamu wa Rais Dk Nchimbi Kwa Watanzania

MSIKITI NA KANISA ZANZIBAR VYAFUNGWA

MWENEZI WA CCM ZANZIBAR AMJIBU OTHMANI MASOUD KWA KINACHOENDELEA HIVI SASA

RAFIKI WA MUUWAJI AFUNGUKA TUKIO ZIMA LA MAUAJI MWANANYAMALA/ALIKUWA AKITAMKA SANA NENO NITAUA

"TANZANIANS, FIGHT FOR A NEW CONSTITUTION": NCHIMBI DROPS A BOMBSHELL

MANSOUR ATAJA KILICHOIFANYA ACT WAZALENDO KUFANIKIWA KATIKA MARIDHIANO

SHEIKH SHAFII;ATAJA SABABU ZA KUSIMAMISHA KWA SHEIKH WALID/SIRI IMEJIFICHA NYUMA YA PAZIA

MAKAME ATOA AGIZO: "USAFI NI JUKUMU LA KILA MWANANCHI!"

WANACHAMA 200 WA CUF PEMBA WAHAMA CHAMA, WATAJA SABABU LUKIKI ZA UAMUZI HUO

Sidee hal gabar u hirgelisay mashruucan? 😮 "How One Woman Built a Big Farm?

Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Hamza Johari, atoa wito huu

What Do Koreans Make with Sweet Potatoes?!

WANANCHI WA IGUGUNO WAZUIA MSAFARA WA KISHOA

Askofu Bagonza Amjibu Dr. Nchimbi, aibua maswali tata ndani ya Serikali.

MASHEHA WAPYA WAAPISHWA MKOWA WA KASKAZINI UNGUJA

NCHIMBI ADDRESSES THE NATION/TOUCHES ON ACTIVISTS AND DISCUSSES THE NEW CONSTITUTION..

DR. NCHIMBI URGES TANZANIANS TO FIGHT FOR A NEW CONSTITUTION, WILL LISSU BE FREED?, MENTIONS MARI...

Massive Fire Erupts at Wildberries Warehouse in St. Petersburg, Russia After Ukrainian Drone Strike

