RAIS MWINYI AWATEMBELEA WAGONJWA WA ZANZIBAR WANAOTIBIWA INDIA

RAIS DKT. MWINYI AWATEMBELEA WAGONJWA WA ZANZIBAR WANAOPATIWA MATIBABU KATIKA HOSPITALI YA MIOT INTERNATIONAL Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amewatembelea wagonjwa kutoka Zanzibar wanaopatiwa matibabu katika Hospitali ya MIOT International, jijini Chennai, nchini India, kupitia udhamini wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. Rais Dkt. Mwinyi amefanya ziara hiyo leo, tarehe 18 Julai 2026, ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kikazi nchini India, kwa lengo la kuwajulia hali wagonjwa hao na kufahamu maendeleo ya matibabu wanayoendelea kupatiwa. Akiwa hospitalini hapo, Rais Dkt. Mwinyi amezungumza na wagonjwa pamoja na familia zao na kupokea maelezo kutoka kwa madaktari kuhusu hali zao za afya, hatua zilizofikiwa katika matibabu na huduma za kibingwa wanazopatiwa. Miongoni mwa wagonjwa waliotembelewa na Rais Dkt. Mwinyi ni Abdallah Bakari Abdallah (18), kijana kutoka Makachu anayepatiwa matibabu katika Kitengo cha Tiba ya Viungo katika hospitali hiyo, ambaye hali yake inaendelea kuimarika. Abdallah ameeleza kufurahishwa na kutimia kwa ndoto yake ya kukutana na Rais Dkt. Mwinyi na kumshukuru kwa kumtembelea, pamoja na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa kumpatia fursa ya kupokea matibabu nchini India. Ziara hiyo pia imeonesha dhamira ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ya kuimarisha ushirikiano na taasisi za afya nchini India, ili kupanua fursa za upatikanaji wa huduma za kibingwa na bobezi kwa wananchi wa Zanzibar. Aidha, Rais Dkt. Mwinyi amepata fursa ya kukutana na madaktari bingwa wanaoendelea na programu ya SET kupitia Mpango wa Mama Samia Scholarship. Rais Dkt. Mwinyi amepokea maelezo kuhusu mafunzo yao, maeneo ya utaalamu wanayosomea na namna maarifa na ujuzi watakaoupata utakavyosaidia kuimarisha utoaji wa huduma za afya nchini. Programu hiyo inalenga kuongeza idadi ya wataalamu wa afya wenye utaalamu wa juu, kuimarisha uwezo wa hospitali nchini kutoa huduma za kibingwa na bobezi, pamoja na kupunguza ulazima wa kupeleka wagonjwa wengi nje ya nchi kwa matibabu.

ASMA MWINYI AENDESHA AMBULANCE KUMPELEKA KIJANA JUMA HOSPOTALI YA LUMUMBA
▶︎

ASMA MWINYI AENDESHA AMBULANCE KUMPELEKA KIJANA JUMA HOSPOTALI YA LUMUMBA

Cooking A Massive Lamb Pilaf For a Mountain Village Feast!
▶︎

Cooking A Massive Lamb Pilaf For a Mountain Village Feast!

RAIS MWINYI: ZANZIBAR KUWA KITUO CHA TEKNOLOJIA NA UBUNIFU
▶︎

RAIS MWINYI: ZANZIBAR KUWA KITUO CHA TEKNOLOJIA NA UBUNIFU

Air Tanzania Cockpit Boeing 767-300 Freighter to Kinshasa
▶︎

Air Tanzania Cockpit Boeing 767-300 Freighter to Kinshasa

SHEIKH WALID AKABIDHI OFISI KWA SHEIKH ABBAS, BAKWATA MKOA DSM
▶︎

SHEIKH WALID AKABIDHI OFISI KWA SHEIKH ABBAS, BAKWATA MKOA DSM

KUMEKUCHA DKT. MWINYI AWAAPISHA MAJAJI WAPYA,  ZANZIBAR!
▶︎

KUMEKUCHA DKT. MWINYI AWAAPISHA MAJAJI WAPYA, ZANZIBAR!

ASMA MWINYI AAHIDI KUMFUTA CHOZI JUMA. ALIYEPOOZA BAADA YA AJALI MBAYA YA VESPA
▶︎

ASMA MWINYI AAHIDI KUMFUTA CHOZI JUMA. ALIYEPOOZA BAADA YA AJALI MBAYA YA VESPA

Why I Want My Kids to Grow Up in South Africa
▶︎

Why I Want My Kids to Grow Up in South Africa

Ni iki kihishe inyuma y'ihomba ry'amahoteli mu Rwanda? | BBC News Gahuza
▶︎

Ni iki kihishe inyuma y'ihomba ry'amahoteli mu Rwanda? | BBC News Gahuza

MO DEWJI ALINITAFUTA NA KUNIPA ZAWADI, MCHUMBA NINAE LAKINI SITAKI KUKURUPUKA
▶︎

MO DEWJI ALINITAFUTA NA KUNIPA ZAWADI, MCHUMBA NINAE LAKINI SITAKI KUKURUPUKA

Dr. Slaa akoleza moto kauli ya Dr. Nchimbi, atoa siri kinachoendelea Nchini.
▶︎

Dr. Slaa akoleza moto kauli ya Dr. Nchimbi, atoa siri kinachoendelea Nchini.

91 Year-Old Grandmother Living Alone In A Mountain Village Forgotten By The World
▶︎

91 Year-Old Grandmother Living Alone In A Mountain Village Forgotten By The World

KUMEKUCHA ZANZIBAR: DKT. MWINYI AZINDUA MABASI YA UMEME, ATAKA VITUO VIKAMILIKE HARAKA
▶︎

KUMEKUCHA ZANZIBAR: DKT. MWINYI AZINDUA MABASI YA UMEME, ATAKA VITUO VIKAMILIKE HARAKA

RAIS SAMIA AZINDUA UJENZI WA MELI ZA MIZIGO KIGOMA
▶︎

RAIS SAMIA AZINDUA UJENZI WA MELI ZA MIZIGO KIGOMA

"Sikutarajia Hii!" TAZAMA Alichokisema Waziri Mkuu Juu ya Tajiri wa Katoro!
▶︎

"Sikutarajia Hii!" TAZAMA Alichokisema Waziri Mkuu Juu ya Tajiri wa Katoro!

IKULU ZANZIBAR: DKT. MWINYI NA UN WOMEN WAKUBALIANA KUIMARISHA UWEZESHAJI WA WANAWAKE NA WASICHANA
▶︎

IKULU ZANZIBAR: DKT. MWINYI NA UN WOMEN WAKUBALIANA KUIMARISHA UWEZESHAJI WA WANAWAKE NA WASICHANA

Rais Samia Suluhu leo aizindua rasmi Taasisi ya Maalim Seif na kutoa hotuba nzito
▶︎

Rais Samia Suluhu leo aizindua rasmi Taasisi ya Maalim Seif na kutoa hotuba nzito

KUMEKUCHA ZANZIBAR! SERIKALI YAZINDUA PROGRAMU MAALUM YA MALEZI YA AWALI YA MTOTO
▶︎

KUMEKUCHA ZANZIBAR! SERIKALI YAZINDUA PROGRAMU MAALUM YA MALEZI YA AWALI YA MTOTO

RC MAKAME ATOA ONYO KALI: ULEVI BARABARANI NI CHANZO CHA AJALI, HESHIMUNI SHERIA
▶︎

RC MAKAME ATOA ONYO KALI: ULEVI BARABARANI NI CHANZO CHA AJALI, HESHIMUNI SHERIA

RIPOTI:IRAN IMEPELEKA WANAJESHI NA MAKAMANDA NCHINI YEMEN ILI KUWAPA NGUVU WAHOUTHI
▶︎

RIPOTI:IRAN IMEPELEKA WANAJESHI NA MAKAMANDA NCHINI YEMEN ILI KUWAPA NGUVU WAHOUTHI

RAIS MWINYI AKUTANA NA JAISHANKAR, AOMBA INDIA KUONGEZA FURSA ZA ELIMU KWA WANAZANZIBAR
▶︎

RAIS MWINYI AKUTANA NA JAISHANKAR, AOMBA INDIA KUONGEZA FURSA ZA ELIMU KWA WANAZANZIBAR

MHE AYOUB: KILIMO CHA MPUNGA KISIMAMIWE KITAALAMU, SI KISIASA
▶︎

MHE AYOUB: KILIMO CHA MPUNGA KISIMAMIWE KITAALAMU, SI KISIASA