MATUMIZI YA TEKNOLOJIA KUKUSANYA TAARIFA ZA VIZAZI NA VIFO
MKOA WA M/ MAGH MATUMIZI YA TEKNOLOJIA KATIKA USAJILI WA VIZAZI NA VIFO 24.06.26 Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala zas Mkoa Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ Mhe Idrissa Kitwana Mustafa .amesema Serikali itaendelea kuimarisha matumizi ya teknolojia katika usajili wa vizazi na vifo ili kuongeza upatikanaji wa takwimu sahihi na utoaji wa huduma bora kwa wananchi. Ameyasema hayo wakati akifungua kikao cha siku moja kwa wadau wa mradi wa kuimarisha mfumo wa usajili wa vizazi na vifo kwa njia ya kidijitali, kilichofanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya Madinat Al Bahri Mbweni Wilaya ya Magharibi B. Mhe.Waziri amesema mradi huo unaumuhimu mkubwa kwani utaunganisha mifumo mbalimbali ya ukusanyaji wa taarifa kutoka ngazi ya Shehia hadi taasisi husika za Serikali, hatua amabayo itaongeza ufanisi katika usimamizi wa taarifa za matukio ya kijamii. Mkurugenzi Mtendaji wa Wakala wa Usajili wa Matukio ya Kijamii Zanzibar, Mohammed Ame Makame amesema mradi huo unalenga kuimarisha usajili wa vizazi na vifo kupitia matumizi ya teknolojia ya kisasa, ikiwa ni pamoja na usambazaji wa vishikwambi (tablets) kwa Masheha ili kurahisisha ukusanyaji na uhifadhi wa taarifa. Akifunga Kikao hicho Salum Shaibu Mussa kwa niaba ya Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ amewaomba wadau walioshiriki kikao hicho kutoa mashirikiano ili kufikia malengo yaliyokusudiwa na Serikali ya kuboresha huduma kwa wananchi wake. Mradi huo ulianza Julai 1, 2025 na unatarajiwa kukamilika Juni 30, 2026, huku ukitarajiwa kuongeza ufanisi wa huduma za usajili na kuimarisha upatikanaji wa takwimu za kuaminika kwa ajili ya maendeleo ya Zanzibar. MWISHO.

HOTUBA YA BAJETI YA MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI KWA MWAKA WA FEDHA 2026/2027

WAZIRI KITWANA AZUNGUMZA NA WAANDISHI WA HABARI SIKU 100 ZA DK. MWINYI KATIKA KIPNDI CHA PILI

JKT Tanzania 0-3 Yanga SC | Highlights | NBC Premier League 30/06/2026

MHE. IDRISSA KITWANA AKIFUNGA MAFUNZO YA VIJANA WA KUJENGA TAIFA

WAZIRI KITWANA AFUNGA MAFUNZO MKUPUO 22/2026

DK. MWINYI AJENGA SKULI YA SEKONDARI KAMA CHUO KIKUU KIFUNDI-PEMBA.

Worst Plane Landing Fails Caught on Camera

A Side of Jamaica The Media Won't Show You!

MAADHIMISHO YA WIKI YA KUWAENZI VIONGOZI WAKUU WA KITAIFA

LAZIMA TUSHIRIKIANE NA WENZETU......MHE HEMED

Sheekada Ninka Soomaaliga Ah Ee Doortay Nolosha Miyiga Dalka Togo 🇹🇬 | Part One

Meet the Former CIA Agent Who Wants to Abolish the CIA

Dkt. Lwaitama akosoa agizo la Waziri Katambi, Akemea mpasuko na Kutoa Ushauri kwa Taifa.

Genius Invention by a 60-Year-Old Plumber! 7 Free Recycling Ideas from Plastic Mesh & Old PVC Pipes

🔴#LIVE: WAZEE WAMTAKA ENG. HERSI YANGA, FEISAL, OKELLO NA MOSSI VITANI/ SIMBA AU YANGA NANI BINGWA?

Nobody Breaks Celebrities Like Rowan Atkinson

Power BI DAX Tutorial for Beginners (2025): Master DAX in ONE Course!

160 KG VILLAGE MONSTER - The ANOMALY Nobody Can Explain - SUPERHUMAN ANDREY SMAEV

