MATUMIZI YA TEKNOLOJIA KUKUSANYA TAARIFA ZA VIZAZI NA VIFO

MKOA WA M/ MAGH MATUMIZI YA TEKNOLOJIA KATIKA USAJILI WA VIZAZI NA VIFO 24.06.26 Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala zas Mkoa Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ Mhe Idrissa Kitwana Mustafa .amesema Serikali itaendelea kuimarisha matumizi ya teknolojia katika usajili wa vizazi na vifo ili kuongeza upatikanaji wa takwimu sahihi na utoaji wa huduma bora kwa wananchi. Ameyasema hayo wakati akifungua kikao cha siku moja kwa wadau wa mradi wa kuimarisha mfumo wa usajili wa vizazi na vifo kwa njia ya kidijitali, kilichofanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya Madinat Al Bahri Mbweni Wilaya ya Magharibi B. Mhe.Waziri amesema mradi huo unaumuhimu mkubwa kwani utaunganisha mifumo mbalimbali ya ukusanyaji wa taarifa kutoka ngazi ya Shehia hadi taasisi husika za Serikali, hatua amabayo itaongeza ufanisi katika usimamizi wa taarifa za matukio ya kijamii. Mkurugenzi Mtendaji wa Wakala wa Usajili wa Matukio ya Kijamii Zanzibar, Mohammed Ame Makame amesema mradi huo unalenga kuimarisha usajili wa vizazi na vifo kupitia matumizi ya teknolojia ya kisasa, ikiwa ni pamoja na usambazaji wa vishikwambi (tablets) kwa Masheha ili kurahisisha ukusanyaji na uhifadhi wa taarifa. Akifunga Kikao hicho Salum Shaibu Mussa kwa niaba ya Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ amewaomba wadau walioshiriki kikao hicho kutoa mashirikiano ili kufikia malengo yaliyokusudiwa na Serikali ya kuboresha huduma kwa wananchi wake. Mradi huo ulianza Julai 1, 2025 na unatarajiwa kukamilika Juni 30, 2026, huku ukitarajiwa kuongeza ufanisi wa huduma za usajili na kuimarisha upatikanaji wa takwimu za kuaminika kwa ajili ya maendeleo ya Zanzibar. MWISHO.