SHIMO NYUMBA YA UHARIBIFU ( DAY ONE) - PASTOR SUNBELLA KYANDO
Mithali 15:11 [11]Kuzimu na Uharibifu vi wazi mbele za BWANA; Si zaidi basi, mioyo ya wanadamu? Kuzimu ni eneo ambalo lipo katika ulimwengu wa roho,kwa maana hiyo hata uharibifu pia ni eneo ambalo lipo katika ulimwengu wa roho,na hadi Neno la Mungu linasema kuwa "vi wazi mbele za Bwana" inamaanisha kuwa ni maeneo ambayo kwa macho ya nyama hayaonekaniki. Neno la Mungu linaendelea kuelezea kuhusu huu uharibifu katika kitabu cha Ayubu; Ayubu 26:6 [6]Kaburi li wazi mbele yake, Uharibifu nao hauna kifuniko. Tofauti ya kaburi na uharibifu ni kuwa kaburi baada ya kuzikiwa hufunikwa lakini uharibifu hauna kifuniko,kwa maana nyingine; kama kaburi ni shimo hata uharibifu nao pia ni shimo kasoro tu halina kifuniko,yaani halifunikwi.Ni sawa chupa ya chai,ukimmiminia mtu mmoja ukimaliza utaifunika lakini kama kuna foleni ya watu wa kuwamiminia kwenye vikombe hautoifunika hadi uwamalize.Kwa maana hiyo uharibifu ni shimo ambalo lipo busy sana,watu wanawekwa hapo sana.Kumbuka UHARIBIFU SIO MATOKEO BALI NI ENEO(LOCATION). Na hili jambo lilimtokea pia Daudi; Zaburi 40:1-2 [1]Nalimngoja BWANA kwa saburi, Akaniinamia akakisikia kilio changu. [2]Akanipandisha toka shimo la uharibifu, Toka udongo wa utelezi; Akaisimamisha miguu yangu mwambani, Akaziimarisha hatua zangu. Mungu baada ya kusikia kilio cha Daudi kitu cha kwanza alichofanya ni kumuhamisha eneo(location) alimokuwemo,yaani shimo la uharibifu.Yeyote anayekuwa ndani ya shimo hakuna kitu atakachokifanya na kikaenda kwa sababu yupo shimoni.Kuna watu kimwili wapo maofisini lakini kiroho wamewekwa kwenye shimo la uharibifu, mshahara wanapata lakini hakuna matunda anayokula kutokana na kazi yake. Biblia inaendelea kusema kuwa "...toka udongo wa utelezi". Kwa maana nyingine hata mtu huyu akijitahidi kutoka kwenye shimo bado atateleza na kuanguka tena,na mara nyingi huumia.Ndio maana kila ambavyo unajitahidi kupiga hatua ndivyo ambavyo unakutana na vitu vya kukuumiza sana na unajikuta unarudi nyuma. Kwa Daudi ilibidi Mungu aingilie kati na kumtoa kwenye hilo shimo, katika sehemu inayofuata tutakuwa na MAOMBEZI na kila shimo la uharibifu ulilowekwa Mungu ataenda kukutoa. UNAWEZA WASILIANA NASI AU KUTUMA SADAKA YAKO KWA NAMBA HII : 0657 173 322 Unaweza kutufuatilia katika mitandao yetu ya kijamii Like our Facebook: / therealityof. . Follow our Instagram: / realityofch. . Subscribe our YouTube: https://www.youtube.com/channel/UC67L... Also Subscribe Roc worshippers youtube channel: / @rocworshipperz and Subscribe Pastor Sunbella Kyando YouTube / @pastorsunbellakyando

NAFASI YA VAZI KATIKA ULIMWENGU WA ROHO - PASTOR SUNBELLA KYANDO

June 4, 2026

🔴LIVE:PASTOR GEORGE MUKABWA | KUJENGA MADHABAHU INAYOMSHUSHA MUNGU.

ENDELEA KUKUSANYA KUNI - PASTOR SUNBELLA KYANDO

JINSI YA KUTEMBEA NA ROHO MTAKATIFU - PASTOR JOSEPH - EIC TV

USINIPITE BWANA - DEEP RELAX SWAHILI WORSHIP SONGS

MAAJABU SABA YA DAMU YA YESU - Innocent Morris

MADHARA YA VYAKULA MTU ANAVYOLISHWA NDOTONI - PASTOR SUNBELLA KYANDO

2.KUSHUGHULIKIA AINA MBALI-MBALI ZA ROHO YA MAUTI

MAARIFA YANAVYOWEZA KUKUSAIDIA KUZISHINDA NGUVU ZA GIZA -PASTOR SUNBELLA KYANDO

MATUNDA YA MUNGU NDANI YA MOYO WA MTU | BISHOP ELIBARIKI SUMBE

MIGUU ILIYOHAMISHWA - PASTOR SUNBELLA KYANDO

ROHO YA MAUTI NA UHARIBIFU (MAOMBEZI) - PASTOR SUNBELLA KYANDO

IMANA YAKOZE BIRIYA NIBINDI IZABIKORA REKA KUGIRA UBWOBA || Pastor SENGA Emmanuel

🔴ፀሎታቹ እዲሰማ ይሄን ያድምጡ! - PROPHET TILAHUN TSEGAYE #jesus #protestantreformation #habesha

Morning Worship Songs 2026 ✝️ Best Praise & Worship Music | Daily Peace Playlist

UMUHIMU NA JINSI YA KUJENGA NGUVU ZAKO ZA NDANI - PST GEORGE MUKABWA | 23/06/2022

HOW THE ALTAR HOLDS A PERSON - PASTOR SUNBELLA KYANDO

MALANGO YA NDOTO YANAVYOTUMIKA NA ADUI (I) - PASTOR SUNBELLA KYANDO

