AJIRA ZA HALMASHAURI NA SEKRETARIETI ZA MIKOA KUOMBWA KUPITIA AJIRA PORTAL

Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma imeendesha mafunzo kwa Maofisa Utumishi na Maofisa TEHAMA kutoka katika Halmashauri na Sekretarieti za Mikoa ya Tabora, Manyara, Kigoma na Lindi. Lengo la mafunzo hayo ni kuwajengea uwezo maofisa hao kuhusu Mchakato wa Ajira ambapo kwa sasa maombi ya Ajira katika Halmashauri na Sekretarieti za Mikoa yataanza kuombwa kupitia mfumo wa Ajira Portal, tofauti na hapo awali ambapo maombi hayo hayakuwa yakifanywa kupitia mfumo huo. Mgeni rasmi katika mafunzo hayo alikuwa ni Kaimu Katibu wa Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma Bwana Innocent Bomani ambaye aliwakilishwa na Naibu Katibu, Mkuu wa Idara ya TEHAMA Mhandisi Samuel Tanguye. Mafunzo hayo yemefanyika mjini Morogoro.