ESRAC: Suluhisho la Haraka kwa Elimu ya Watoto Wenye Ulemavu

Agness ni mwanafunzi mwenye ulemavu wa miguu, kutokana na tatizo hilo amekuwa akikabiliwa na kushindwa kuhudhuria shule ipasavyo kwa sababu ilimlazimu mama yake ambebe kumpeleka shule kila siku. Inapotokea mama yake ameshindwa kumpeleka shule basi ilikuwa ni ngumu kwa Agness kufika shule. Hali hiyo ilibadilika baada ya Sense International Tanzania kumpatia Agness kitimwendo. Makala hii inazungumzia maisha ya Agness kabla ya kupata kiti na baada ya kupata kiti.