RAIS DKT. MWINYI AZINDUA MABASI YA UMEME, AITAKA ZSSF IKAMILISHE VITUO VYA KISASA HARAKA
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ameutaka Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar (ZSSF) kukamilisha kwa haraka ujenzi wa vituo vya kisasa vya mabasi vinavyotekelezwa chini ya Mradi wa Mabasi ya Umeme ili wananchi waanze kunufaika kikamilifu na huduma hiyo. Dkt. Mwinyi ametoa kauli hiyo leo, Julai 23, 2026, wakati wa ufunguzi wa Kituo cha Mabasi Malindi na uzinduzi rasmi wa huduma za usafiri wa umma kwa kutumia mabasi ya umeme uliofanyika Malindi, Mkoa wa Mjini Magharibi. Amesema mradi huo unalenga kuboresha huduma za usafiri wa umma kwa kuwapatia wananchi usafiri wa kisasa, salama na wa uhakika, sambamba na kuimarisha mfumo wa usafiri na kuongeza hadhi ya mji wa Zanzibar. Aidha, amesema Serikali imejipanga kuhakikisha vyombo vya usafiri vinavyotoka maeneo ya nje ya mji vinaishia katika vituo vitakavyojengwa pembezoni mwa mji, huku mabasi ya umeme yakitoa huduma ndani ya Mkoa wa Mjini Magharibi. Rais pia ameipongeza ZSSF kwa kukamilisha kwa wakati ujenzi wa uwanja wa michezo kwa watoto uliojengwa karibu na Kituo cha Mabasi Malindi, akieleza kuwa utatoa mazingira salama kwa watoto kushiriki michezo na shughuli za kijamii. Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa ZSSF, Nassor Shaaban Ameir, amesema mradi huo unatarajiwa kuzalisha ajira nyingi kwa vijana kupitia huduma mbalimbali zitakazohusiana na uendeshaji wa mabasi ya umeme, ikiwa ni sehemu ya mchango wa mfuko huo katika kukuza uchumi wa Zanzibar. Naye Waziri wa Fedha na Mipango Zanzibar, Dkt. Juma Malik Akil, amesema mradi huo unatekeleza kwa vitendo maono ya Rais Dkt. Hussein Ali Mwinyi ya kurejesha na kuboresha huduma za usafiri wa umma kwa viwango vya kisasa. Hafla hiyo pia iliambatana na uzinduzi wa kadi maalumu za usafiri, zikiwemo kadi za dhahabu kwa wanafunzi, kadi nyeusi kwa wazee na kadi za buluu kwa abiria wengine. #Zanzibar #MabasiYaUmeme #Malindi #ZSSF #DktHusseinAliMwinyi #Usafiri #Miundombinu #AsamOnlineTV #SisiNiJamii

🔴 #ZBCLIVE :- UZINDUZI WA KITUO CHA MABASI YA UMEME, MALINDI ZANZIBAR

MLANGO WAVUNJWA, POLISI WASIMAMIA MAKABIDHIANO OFISI YA SHEIKH WA MKOA WA SINGIDA

UTAPENDA" RAIS MWINYI AMTEMBELEA KIJANA WA MAKWACHU INDIA

RASMI: NAULI ZA DALADALA ZAPANDA KUTOKA SH. 500 HADI 700 KUANZIA AGOSTI 1

Why AIR TANZANIA Might Surprise You 🇹🇿

ZANZIBAR HII HUWEZI KUAMINI

KUPANDA KWA BEI ZA NAULI ZANZIBAR WANANCHI WAJA NA YAO MAPYAA

RAIS MWINYI AJIBU MASHAMBULIZI KUHUSU MIRADI ANAYOIJENGA ZANZIBAR

IRAN IMEWEKA NGUMU KWA TRUMP | HATAKI MAZUNGUMZO, WANATUPIANA MPIRA KILA UPANDE UNARUSHA MANENO

MAWAZIRI WA SMZ WASHUKA MASHAMBANI, WAWEKA MIKAKATI YA MAPINDUZI YA KILIMO

EXCLUSIVE: KWA MARA YA KWANZA MANDIETA AELEZEA KWA UNDANI UKARIBU WAKE NA MAREHEMU JEBA

TAZAMA SOKA LA COACH MANQOBA MNGQITHI SIKU YA KWANZA KAZINI

Trump administration signs nuclear agreement with Saudi Arabia | What to know

Heche: Hakuna Mazungumzo Yatakayofanyika Bila Mwenyekiti Kuwa Nje

ALI KARUME AIBUA MAPYA, ASEMA CCM HAIJAWAHI KUSHINDA UCHAGUZI ZANZIBAR, WANAKAA MADARAKANI KWA UBABE

TUFUNUWE KITABU (SILSILA 25): Zanzibar: The Last Years of the Protectorate cha Maulid Mshangama

Trump adds new condition to Saudi nuclear deal

OMO makes clear its position on land and rights of Zanzibari | ZANZIBAR DECIDES 2025

UKAGUZI WA STAND YA NGANGAMFUMUNI

