Uwezo Kidogo Kama Sindano ya Kushona Nguo / Kufaa Mara Kumi Zaidi | Rev. Dr. Eliona Kimaro

KIJITONYAMA LUTHERAN CHURCH: IBADA YA HITIMISHO - MAFUNGO WA SIKU 40: 13/ 12/ 2024 13/ 12/ 2024 MAFUNGO YA SIKU 40, SIKU YA 40 KICHWA CHA SOMO: ''WEKEZA KWENYE UWEZO WAKO" "INVEST IN YOUR CAPABILITY" NENO KUU : Waamuzi 6 : 14 ENENDA KWA UWEZO WAKO HUU UJUMBE WA LEO: WEKEZA KWENYE UWEZO WAKO (INVEST IN YOUR CAPABILITY) UWEZO KIDOGO KAMA SINDANO YA KUSHONA NGUO (KUFAA MARA KUMI ZAIDI) Matendo 9 : 36 - 43 Danieli 1 : 17 - 21 Matendo 9 : 36 - 43 36 Na mwanafunzi mmoja alikuwako Yafa, jina lake Tabitha, tafsiri yake ni Dorkasi (yaani paa); mwanamke huyu alikuwa amejaa matendo mema na sadaka alizozitoa. 37 Ikawa siku zile akaugua, akafa; hata walipokwisha kumwosha, wakamweka orofani. 38 Na kwa kuwa mji wa Lida ulikuwa karibu na Yafa, nao wanafunzi wamesikia ya kwamba Petro yuko huko, wakatuma watu wawili kwake, kumsihi na kusema, Usikawie kuja kwetu. 39 Petro akaondoka akafuatana nao. Alipofika, wakampeleka juu orofani wajane wote wakasimama karibu naye, wakilia na kumwonyesha zile kanzu na nguo alizozishona Dorkasi wakati ule alipokuwa pamoja nao. 40 Petro akawatoa nje wote, akapiga magoti, akaomba, kisha akaelekea yule maiti, akanena, Tabitha, ondoka. Naye akafumbua macho yake, na alipomwona Petro akajiinua, akaketi. 41 Akampa mkono, akamwinua; hata akiisha kuwaita wale watakatifu na wajane akamweka mbele yao, hali yu hai. 42 Ikajulikana katika mji mzima wa Yafa; watu wengi wakamwamini Bwana. 43 Basi Petro akakaa siku kadha wa kadha huko Yafa, nyumbani mwa mtu mmoja, jina lake Simoni, mtengenezaji wa ngozi. Danieli 1 : 17 - 21 17 Basi, kwa habari za hao vijana wanne, Mungu aliwapa maarifa na ujuzi katika elimu na hekima; Danieli naye alikuwa na ufahamu katika maono yote, na ndoto. 18 Hata mwisho wa siku zile alizoziagiza mfalme za kuwaingiza, mkuu wa matowashi akawaingiza mbele ya mfalme Nebukadreza. 19 Naye mfalme akazungumza nao; na miongoni mwao wote hawakuonekana waliokuwa kama Danieli, na Hanania, na Mishaeli, na Azaria; kwa hiyo wakasimama mbele ya mfalme. 20 Na katika kila jambo la hekima na ufahamu alilowauliza mfalme, akawaona kuwa walifaa mara kumi zaidi ya waganga na wachawi waliokuwa katika ufalme wake. 21 Tena, Danieli huyo akadumu huko hata mwaka wa kwanza wa mfalme Koreshi. FALSAFA PANA 1. LEARN TO KEEP PEOPLE DEPENDENT ON YOU.... (JIFUNZE KUWAFANYA WATU WAKUTEGEMEE... HAKIKISHA UNATEGEMEWA) 2. MAKE THEM WANT TO FOLLOW YOU.... (WAFANYE WATU WAKUFUATE POPOTE ULIPO) Mhubiri: Rev. Dr. Eliona Kimaro Kwa maombi na ushauri : Mch. Kiongozi: Dr. Eliona Kimaro Simu: +255 655 516 053, +255 754 516 053