MKULIMA TARIME ASIMULIA ANAVYOINGIZA MAMILIONI YA PESA KUPITIA KILIMO IKOLOJIA.
Katika kijiji Kewamamba Kata ya Kiore wilayani Tarime mkoani Mara, mkulima Nuhu ameendelea kuwa mfano wa mafanikio kupitia kilimo ikolojia na uzalishaji wa mbegu za asili zinazowasaidia wakulima wengi ndani na nje ya jamii yake. Kupitia kilimo hicho, Nuhu huzalisha mazao mbalimbali ya asili pamoja na mbegu anazowagawia na kuwauzia wakulima wengine ili kuwahamasisha kutumia mbegu salama na zinazotunza mazingira,ambapo mpaka sasa ameshawapatia mbegu za asili wakulima zaidi ya mia tano katika kijiji chake na maeneo ya jirani. Nuhu amesema kilimo ikolojia kimembadilishia maisha kwa kiasi kikubwa kwani mbali na kulisha familia yake chakula safi na salama kisicho na kemikali,kulinda mazingira,pia kimemwezesha kusomesha watoto wake, kujenga nyumba nzuri ya kuishi na kuboresha maisha ya familia yake kwa ujumla. Mkulima huyu hutumia mbolea za asili kama samadi badala ya pembejeo za viwandani ili kulinda afya ya udongo na mazingira. Kupitia mauzo ya mazao ya kiikolojia anayolima, Nuhu anaingiza zaidi ya shilingi milioni kumi kila mwaka, jambo ambalo limekuwa chachu kwa wakulima wengine kuanza kuona thamani ya kilimo kinachozingatia afya ya binadamu na uhifadhi wa mazingira. Mbegu za asili anazozalisha pia zimeendelea kusaidia wakulima wengi kupata mazao bora na endelevu. Nuhu pia amekishukuru Kituo cha Mogabiri kilichopo wilayani Tarime pamoja na mradi wa Agro Kilimo unaoratibiwa na taasisi ya IDP kwa kumpatia elimu ya kutosha kuhusu kilimo ikolojia na kumkutanisha na wakulima wengine ambapo ameweza kujipatia ujuzi zaidi. Aidha Bwana Nuhu ametoa wito kwa wakulima wengine kujikita katika kilimo ikolojia ili waweze kunufaika kiafya,kiuchumi na kutunza mazingira. #agroecologyrightnow #sustainablefoodsystems #organic #smartfarming

Earn Ksh 2 Million Per Acre with Hybrid Sukuma Wiki: A Farmer's Success Story

KUTOKA NDULI HADI KIDAMALI, DK BASHIRU ASHUHUDIA UWEKEZAJI MKUBWA SEKTA YA MAZIWA IRINGA

Idp yawaleta pamoja wadau wa kilimo Ikolojia kupitia mradi wa Agro Kilimo.

FORI Yafunga Pazia la miaka mitatu ,ikiacha Urithi wa Maarifa,Ustahimilivu na mafanikio Mashambani.

Teknolojia ya DNA Yafichua Chanzo cha Uharibifu wa Mazao Kilolo

Sababu Inayowafanya Wasomi Wengi Kushindwa Biashara Uraiani

Fahamu siri ya kutokuzeeka mapema.

MWALIMU ASIMULIA ALIVYOKATWA MKONO NA MUMEWE, WATOTO WAKE WAONE VIDOGOLE VILIVYOKATWA, WANAFUNZI

Mtendaji anayenufaika na kilimo cha vitunguu Lindi.

Mbegu za Asili suluhisho la gharama kubwa za kilimo,afya na mazingira.

መስኖ ለወጣቶች - ወደ ገጠር |ወደ ገጠር| ETV |EBC |ETHIOPIAN

Hii hapa siri ya Lishe bora na faida kubwa kibiashara.Ni kilimo Ikolojia.

How Traore is Magically Growing Real Apples in Desert?

Never Buy a Water Pump Again! A 65-Year-Old Plumber Made His Own Water Pump Using PVC Pipes | Update

"DON'T THREATEN ME": HECHE RESPONDS TO MINISTER KATAMBI IN MPANDA, Reveals the Whole Story

KILIMO IKOLOJIA CHATINGA MASOKONI NA MINADANI

Ushirikishwaji wa wadau wa kilimo Ikolojia,msingi wa viwango bora na Masoko endelevu.

Kutoka Shambani hadi Mezani,hii ndio siri ya afya njema.

Pour Cement into Pallets and see what most people don't even imagine happens! Creation Daily

