Barikiwa kupitia ushuhuda - PASTOR ELIUS MASHA

Ujumbe wa Baraka: Mungu akujaze Roho wake Mtakatifu, akupe ujasiri wa kusimama katika kweli, afungue milango iliyofungwa mbele yako, na akutie nguvu katika kila jambo unalopitia. Kama alivyotikisa mahali walipokuwa wanaomba, na atikise kila kikwazo kinachosimama dhidi ya kusudi lake katika maisha yako. Uishi katika ushindi, amani, na neema ya Mungu kila siku. Amina. 🙏🏽 Neno la Kutafakari: "Nao walipokwisha kumwomba Mungu, mahali pale walipokusanyika pakatikisika; wote wakajazwa Roho Mtakatifu, wakalinena neno la Mungu kwa ujasiri." (Matendo 4:31)