11. ULIACHA MBINGUNI By Tabernacle de Likasi (Album Merci Seigneur)

1. Uliacha mbinguni na utukufu Kufika dunia kwa mimi ; Saa ulipozaliwa kwa Betelehemu Na fasi hukuipata. 2. Malaika za mbingu walikusifu Mufalme mukubwa wa mbingu; Ulijifanya kuwa bila utukufu Na ulijinyenyekeza. 3. Mbweha wana matundu, na ndege vile Kwa miti vioto viao; Kwawe Mwana wa Mungu sanduku ya nyama Ni kama kitanda chako. 4.Ulikuja na neno lenye uzima Kwa kutufungua sisi; Watu walikufunga na kukupeleka Kwa kufa musalabani. 5. Kisha siku nyingine utarudia Mufalme wa utukufu; Utani-ita kwako ukiniambia : "Mbinguni nafasi iko". Chorus Ingia moyoni mwangu Bwana nina nafasi kwawe, Ingia moyoni mwangu Bwana nina nafasi kwawe.