Gilbert Godfrey.Neno ni Yesu.

Neno ni Yesu , Yesu ni Neno la Mungu . Neno hili limeumba vyote ,Wala pasipo Neno hakikufanyika chochote kilichofanyika. ndani ya Neno Hilo ndimo Kuna uzima na uzima huo ndiyo Nuru halisi ya watu. ukimwamini Leo Huyu Neno ambaye ni Bwana Yesu ,hautatembea kamwe gizani. Yohana 1:1-5 Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu. Huyo mwanzo alikuwako kwa Mungu. Vyote vilifanyika kwa huyo; wala pasipo yeye hakikufanyika cho chote kilichofanyika. Ndani yake ndimo ulimokuwa uzima, nao ule uzima ulikuwa nuru ya watu. Nayo nuru yang’aa gizani, wala giza halikuiweza. Usiendelee kukaa gizani ,Yesu ni Nuru Yako halisi.