VETA TUPO NANENANE MTAA WA MSABAHA, UWANJA WA JOHN MWAKANGALE, JIJINI MBEYA

Msimu wa Nanenane ndio huooooo unaendelea! Na kama kawaida VETA tupo Mbeya Uwanja wa John Mwakangale banda lipo mtaa wa Msabaha uwanjani limesheheni mambo kibao. Tembelea banda la VETA ujipatie fomu ya kujiunga na mafunzo ya ufundi stadi, ujionee ubunifu tofautitofauti kwa ajili ya kuboresha shughuli za kilimo na upate huduma mbalimbali ikiwemo matengenezo ya simu za mkononi na huduma za ususi na urembo.